Sunday , 3 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Spika Ndugai azuia wakurugenzi wa Uchaguzi kuguswa
Habari za Siasa

Spika Ndugai azuia wakurugenzi wa Uchaguzi kuguswa

Spread the love

SPIKA wa Bunge Job Ndugai amemzuia Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Susan Kolimba kujibu maswali ya Mbunge wa Kitambile Masoud Abdallah Salim ambapo mojawapo lilihoji kuwa, lini serikali itapeleka mswada bungeni wa kubadili sheria inayoruhusu Wakurugenzi wa Halmashauri kuwa wasimamizi wa uchaguzi. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Salim aliuliza amswali hayo leo tarehe 13 Septemba 2018 bungeni jijini Dodoma, ambapo amedai kuwa, kitendo cha wakurugenzi wa halmashauri kuwa wasimamizi wa uchaguzi, kinaminya uhuru wa demokrasia kutokana kwamba wakurugenzi hao ni makada wa chama tawala nchini CCM na hivyo ikifika kipindi cha uchaguzi wanakuwa marefa wa kuisaidia CCM kupata ushindi.

Mbunge huyo alilielekeza maswali mawili ya nyongeza katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, ambapo swali lilingine aliihoji wizara hiyo kwamba, kwa nini serikali imeshindwa kudhibiti mfumuko wa bei ya sukari kitendo kinachochangia ugumu wa maisha kwa wananchi.

Baada ya Salim kuuliza maswali hayo, Spika Ndugai aliyakataa maswali hayo akisema kuwa hayaendani na swali lake la msingi pamoja na kuuliza katika wizara isiyo sahihi, lakini pia kuhusu swali lake mfumuko wa bei ya sukari, alisema litajibiwa na Waziri wa Viwanda na Biashara, Charles Mwijage.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Biteko aagiza wakurugenzi TANESCO kukemea rushwa kwenye maeneo yao

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Uongozi wa Samia kuendelea hadi 2030

Spread the loveKWETU sisi tuliowahi kusoma sekondari, iwe O levo au A...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Bado askari wastaafu wanaonewa

Spread the loveRAIS wangu Samia Suluhu Hassan tunaendelea kumshukuru Mungu kwamba wote...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Tunastawisha ufisadi na kuchukia matunda yake

Spread the loveBUNGE la Jamhuri linaloendelea mjini Dodoma, kwa wiki nzima limetawaliwa...

error: Content is protected !!