Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wakandarasi wanaichonganisha serikali na wananchi
Habari Mchanganyiko

Wakandarasi wanaichonganisha serikali na wananchi

Suleiman Jaffo, Naibu Waziri wa Nchi, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Spread the love

NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR – TAMISEMI) Suleiman Jafo amewaambia wakandarasi kutotimiza wajibu wao na kukamilisha kwa muda muafaka miradi wanayopewa na mamlaka za serikali ni kuwachonganisha kwa wananchi, anaandika Dany Tibason.

Mbali na kuwagombanisha na wananchi lakini kitendo cha kuingiza ubabaishaji katika utendaji wao wa kazi wanasababisha kuchelewesha maendeleo kwani miradi hiyo ikikamilika inachochea maendeleo.

Akizungumza katika uzinduzi wa mradi wa maji katika kijiji cha Wilunze wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma, Jafo amesema mkandarasi yeyote atakayepewa tenda ya mradi katika halmashauri yoyote nchini na asiitekeleze kwa wakati hataweza kupewa tenda mahali popote pale nchini.

“Kumekuwa na uzembe kwa wakandarasi nchini, mkandarasi anapewa kazi ya kujenga daraja, kujenga visima vya maji, barabara au mradi mwingine wowote katika halmashauri, badala ya kutekeleza mradi huo kwa wakati ili wananchi waendelee kupata huduma hiyo, yeye analeta uzembe na ubabaishaji, mtu wa namna hiyo hatutamvumilia katika serikali hii,” amesema Jafo.

Aidha, aliwataka wanakijiji wa Wilunze kuulinda mradi huo wa maji kwa kila mmoja kuwa msimamizi wa mradi na kuutaka uongozi wa kijiji kuhakikisha kuwa kinaundwa chombo cha watumiaji wa maji kijijini hapo ambacho kitakuwa na wajibu wa kusimamia mradi huo.

Mradi wa maji wa kijiji cha Wilunze uliozinduliwa leo ni mmoja kati ya miradi ya maji ya vijiji 10 inayojengwa wilayani Chamwino kupitia Programu ya Maji Vijijini. Mradi huo uliojengwa na Mkandarasi M/S Kijima Contractors akisimamiwa na Ofisi ya Mhandisi wa Maji Chamwino umegharimu jumla ya sh. 347,909,621.

Kwa upande wake Mbunge wa Chilonwa, Joel Mwaka amemshukuru naibu waziri na serikali kwa ujumla kwa kuwapatia huduma ya maji safi wananchi wake na kuwasisitiza wananchi kuuliunda mradi huo kwa hali na mali kwani umeigharimu serikali kiasi kikubwa cha fedha katika utekelezaji wake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!