Monday , 5 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Wakandarasi wanaichonganisha serikali na wananchi
Habari Mchanganyiko

Wakandarasi wanaichonganisha serikali na wananchi

Suleiman Jaffo, Naibu Waziri wa Nchi, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Spread the love

NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR – TAMISEMI) Suleiman Jafo amewaambia wakandarasi kutotimiza wajibu wao na kukamilisha kwa muda muafaka miradi wanayopewa na mamlaka za serikali ni kuwachonganisha kwa wananchi, anaandika Dany Tibason.

Mbali na kuwagombanisha na wananchi lakini kitendo cha kuingiza ubabaishaji katika utendaji wao wa kazi wanasababisha kuchelewesha maendeleo kwani miradi hiyo ikikamilika inachochea maendeleo.

Akizungumza katika uzinduzi wa mradi wa maji katika kijiji cha Wilunze wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma, Jafo amesema mkandarasi yeyote atakayepewa tenda ya mradi katika halmashauri yoyote nchini na asiitekeleze kwa wakati hataweza kupewa tenda mahali popote pale nchini.

“Kumekuwa na uzembe kwa wakandarasi nchini, mkandarasi anapewa kazi ya kujenga daraja, kujenga visima vya maji, barabara au mradi mwingine wowote katika halmashauri, badala ya kutekeleza mradi huo kwa wakati ili wananchi waendelee kupata huduma hiyo, yeye analeta uzembe na ubabaishaji, mtu wa namna hiyo hatutamvumilia katika serikali hii,” amesema Jafo.

Aidha, aliwataka wanakijiji wa Wilunze kuulinda mradi huo wa maji kwa kila mmoja kuwa msimamizi wa mradi na kuutaka uongozi wa kijiji kuhakikisha kuwa kinaundwa chombo cha watumiaji wa maji kijijini hapo ambacho kitakuwa na wajibu wa kusimamia mradi huo.

Mradi wa maji wa kijiji cha Wilunze uliozinduliwa leo ni mmoja kati ya miradi ya maji ya vijiji 10 inayojengwa wilayani Chamwino kupitia Programu ya Maji Vijijini. Mradi huo uliojengwa na Mkandarasi M/S Kijima Contractors akisimamiwa na Ofisi ya Mhandisi wa Maji Chamwino umegharimu jumla ya sh. 347,909,621.

Kwa upande wake Mbunge wa Chilonwa, Joel Mwaka amemshukuru naibu waziri na serikali kwa ujumla kwa kuwapatia huduma ya maji safi wananchi wake na kuwasisitiza wananchi kuuliunda mradi huo kwa hali na mali kwani umeigharimu serikali kiasi kikubwa cha fedha katika utekelezaji wake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga 60 milioni kujenga machinjio ya kisasa

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma Imetenga kiasi cha Tshs Miloni 60...

Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa...

Habari Mchanganyiko

Bandari ya Kigoma kuongezewa uwezo wa kutoa huduma zake

Spread the love  SERIKALI kupitia mamlaka ya Bandari nchini (TPA), imewekeza takribani...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kifo cha mwanafunzi UDOM: Tume yamsafisha naibu waziri

Spread the loveTUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini (THBUB),...

error: Content is protected !!