Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wagombea urais CUF kujulikana Julai 27
Habari za Siasa

Wagombea urais CUF kujulikana Julai 27

Prof. Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa CUF
Spread the love

WAGOMBEA Urais wa Tanzania na Zanzibar wa Chama cha Wananchi (CUF), katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020, kujulikana Jumatatu ya tarehe 27 Julai 2020. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Ratiba hiyo imetolewa leo Alhamisi tarehe 16 Julai 2020, na Juma Kilaghai, Mkurugenzi wa Mipango na Uchaguzi CUF, wakati anazungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam.

Kilaghai amesema, wagombea hao watapatikana baada ya wajumbe wa mkutano mkuu, kuchagua jina moja kati ya majina ya wanachama waliojitokeza kutia nia kugombea nafasi hizo.

“CUF itafanya mkutano mkuu wa taifa maalum kwa ajili ya uchaguzi wa wagombea, tarehe 27 Julai 2020,” amesema Kilaghai.

Hadi sasa, Chief Lutalosa Yemba, mwanachama pekee wa CUF aliyejitosa kugombea urais wa Tanzania huku urais wa Zanzibar wakijitokeza watia watano.

Chifu Lutayosa Lyemba

Hata hivyo, bado dirisha la uchukuaji na urejeshaji fomu za kugombea urais wa Tanzania na Zanzibar ndani ya CUF litahitimishwa tarehe 18 Julai 2020.

Waliojitosa ni, Faki Suleiman Khatibu, aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu CUF Zanzibar. Abbas Juma Mhunzi, aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa CUF Zanzibar, Mhandisi Mohamed Habib Mnyaa, Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki.

Mussa Haji Kombo na Rajab Mbarouk, ni wanachama wa CUF waliojitokeza kutia nia kugombea Urais wa Zanzibar katika uchaguzi huo.

Kwa upande wa mchakato wa kuwapata wagombea ubunge, uwakilishi na udiwani katika uchaguzi huo, unatarajiwa kukamilika tarehe 24 hadi 25 Julai 2020, baada ya zoezi la uchukuaji na urejeshaji fomu kufungwa tarehe 18 Julai 2020.

“Mchakato wa ubunge, uwakilishi, udiwani na viti maalum unaendelea. Kura za maoni zimeanza siku tano zilizopita, tumepata asilimia 70 ya wagombea wote kwa upande wa bara. Tarehe 18 Julai zoezi litakamilika, wagombea wanapitishwa na Baraza Kuu la Uongozi,” amesema Kilaghai.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!