Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Usaliti Chadema watibua uchaguzi Meya
Habari za SiasaTangulizi

Usaliti Chadema watibua uchaguzi Meya

Mch. Peter Msigwa, Mbunge wa Iringa Mjini
Spread the love

HOFU ya usaliti ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), mkoani Iringa imekwaza kufanyika kwa uchaguzi wa Naibu Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Hatua hiyo imetokana na Chadema kupendekeza utaratibu wa upigaji kura kwa kuweka alama zaidi ya vema kwenye karatasi ya kura. Uchaguzi huo ulitakiwa kufanyika jana tarehe 16 Oktoba 2019, umeahirishwa.

Chadema Iringa kwenye uchaguzi, iliweka utaratibu wa kuweka alama zaidi ya vema kutokana na hofu ya kusalitiwa na baadhi ya wapiga kura wake, wanaodaiwa kupokea ‘mlungula’ kutoka CCM.

Katika Halmashauri hiyo, idadi ya madiwani wa Chadema na wabunge wao ni 14 ambapo ni idadi sawa na wale wa CCM ambao ni 14.

Taarifa za ndani zinaeleza kwamba, CCM imeweka mtego kwa baadhi ya wapiga kura wa Chadema, kwamba wakipata kuta hata moja kutoka upande wa pili (Chadema), itawawezesha kuwa na kura 15 huku Chadema wakibaki na kura 13 jambo litalowawezesha (CCM) kushinda uchaguzi huo.

Kumea kwa hofu hiyo, ndio kuliisukuma Chadema kuibua na mkakati wa kulinda kura kwa kuwataka wajumbe wake (wapiga kura), kuweka alama zaidi ya vema ili kuwatambua kama watasaliti kwa kuwapigia kura CCM ama kuharibu kura kwa kusudi.

Mjadala wa hoja ya Chadema ndio uliovuruga utaratibu wa uchaguzi na kusababisha Hamid Njovu, msimamizi wa uchaguzi katika halmashauri hiyo kuahirisha uchaguzi.

“Sasa naahirisha baraza hili mpaka wakati mwingine, wajumbe wote nawaomba mkasome sheria na kanuni za uchaguzi ili kukwepa kukiuka masharti,” amesema Njovu wakati akiahirisha uchaguzi huo.

Amesema, hawezi kuruhusu uchaguzi huo kufanyika kwa kuwa, madiwani ambao kisheria ndio wapigakura, waliibua mjadala kuhusu matumizi ya kanuni za upigaji kura.

“Kuna tatizo katika kuelewa kanuni,” amesema Njovu na kuongeza “manapaswa mkasome kanuni ili mzielewe vizuri.”

Peter Msigwa, Mbunge wa Iringa Mjini kupitia Chadema amesema, wanataka kuwajua wasaliti kwenye uchaguzi huo na hivyo, wamependekeza namna ambayo itawawezesha kuwajua.

“Tulichokitaka sisi ni kwamba wasituwekee masharti ya namna ya mtu apige kura vipi,” amesema Mchungaji Msigwa na kuongeza “Sisi Chadema tulikubaliana wote tuweke alama itakayomuonesha kila mmoja wetu amepiga kura, ili tumjua atakayesaliti.”

Njovu ameahirisha uchaguzi huo bila kutaja tarehe ya kufanyika, baadhi ya wabunge wa CCM wamepongeza uamuzi wa kuahirisha uchaguzi huo huku wakisisitiza kura ni siri na kwamba itabaki hivyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!