Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Udhaifu vituo vya utafiti wamuinua Sugu bungeni
Habari za Siasa

Udhaifu vituo vya utafiti wamuinua Sugu bungeni

Spread the love

MBUNGE wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (Sugu) kutoka Chadema ameiomba serikali kueleza ni lini itatenga fedha za kutosha kwa ajili ya kufufua vituo vya utafiti kama vile Chuo cha Utafiti kilichopo Uyole, Mbeya. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).

Akiuliza swali la nyongeza bungeni Mbilinyi amesema kuwa, kwa sasa Chuo cha Uyole kinakabiliwa na miundombinu pamoja na ufinyu wa bajeti.

Amehoji, lini serikali itaweza kuweka mipango ya kuongeza bajeti ili kuweza kufanya chuo hicho kuwa na miundombinu pia kukiongezea bajeti ili kiweze kufanya vizuri zaidi.

Katika swali la msingi la Martin Msua, Mbunge wa Mbinga Vijijini (CCM) aliyetaka kujua ni lini serikali ilifanya utafiti wa gharama za uzalishaji wa kahawa wilayani Mbinga kwa mara ya mwisho.

Akijibu maswali hayo Omar Mgumba, Naibu Waziri wa Kilimo amesema, serikali ilipeleka mswada wa Sheria bungeni na kuunda vituo 16 ambapo kila kituo kitakuwa kikifanya utafiti wa mazao mawili tu.

Mgumba amesema, lengo la kufanya kila kituo kufanya utafiti wa ni kufanya vituo hivyo visiweze kulemewa katika utendaji wao wa kazi.

Akizungumzia suala la kuwezesha kituo kikubwa cha Utafiti cha Uyole amesema, katika bajeti ya mwaka wa fedha 2019/20 watakitengea fedha chuo hicho.

Mgumba amesema kuwa, serikali katika mwaka wa fedha 2015/2016 kupitia taasisi ya Utafiti wa Kahawa Tanzania (TaCRI) imefanya utafiti wa uzalishaji wa kahawa katika wilaya saba;- Mbinga, Mbozi, Tarime,Rombo, Muleba, Karagwe na Buhigwe.

Amesema, utafiti uliofanywa na TaCRI kwa wakulima wa kahawa aina ya Arabca unaonesha gharama za uzalishaji wa aina bora za kahawa zenye ukinzani wa magonjwa Sh. 2.1 Mil kwa heka sawa na wastani wa Sh. 843.4 kwa kilo zenye tija ya wastani wa kilo 2662 kwa hekta.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!