Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Tundu Lissu amchongea Ngeleja Takukuru
Habari za SiasaTangulizi

Tundu Lissu amchongea Ngeleja Takukuru

Tundu Lissu, Rais wa TLS
Spread the love

TUNDU Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki na Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) amemuwakia William Ngeleja, Mbunge wa Sengerema baada ya kurudisha fedha za Escrow zinazodaiwa kutakatishwa, anaandika Irene Emmanuel.

Lissu amedai kuwa, Ngeleja ni sehemu ya mafisadi wanaotumia madaraka vibaya hivo anatakiwa kushtakiwa pamoja na wengine wote walionufaika na pesa hizo, kurudisha fedha Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) si suluhu kwani sio hao waliompatia fedha hizo apo  awali.

Ameeleza kuwa, kutokana na maelezo yake yanaonyesha yeye ni mla rushwa na muongo, sakata hilo ni la muda mrefu sasa na si kama amejua juzi.

“Kusema  alijua juzi kuwa fedha hizi ni kashfa, ni kutundanganya, anatakiwa kukamatwa na kushtakiwa,” amesema Lissu na kuongeza: “Nchi hii ukikamatwa umeiba ndiyo kesi imeishia hapo?Sheria ni kuwa ukikamatwa umeiba unafikishwa kwenye vyombo vya dola ukakutwa na hatia unafungwa na fedha kurudishwa.”

Aliongeza kuwa, wote walionufaika na fedha hizo wanapaswa kuwajibishwa na kumtaka rais achukue hatua kuanzia aliyeruhusu fedha hizo zitoke, kwani naye analeta maswali mengi.

Ngeleja aliwahi kuwa mwenyekiti wa kamati ya bunge na kuondolewa mwaka 2014 baada ya sakata hilo, na juzi ameripotiwa kurudisha fedha TRA alizopewa na James Rugemalira, fedha zinazodaiwa kutakatishwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!