Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Tume ya Uchaguzi yatangaza uchaguzi Jimbo la Nassari
Habari za SiasaTangulizi

Tume ya Uchaguzi yatangaza uchaguzi Jimbo la Nassari

Spread the love

MWENYEKITI wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Semistocles Kaijage ametangaza uchaguzi mdogo wa Jimbo la Arumeru Mashariki. Anaripoti Hamisi Mguta … (endelea).

Akitoa taarifa hiyo Jaji Kaijage amesema kuwa uchaguzi huo utafanyika tarehe 19, Mei 2019 na fomu za wagombea zitatolewa kati ya Aprili 15 au 19 na uteuzi wa wagombea utafanyika Aprili 19 mwaka huu.

“Kwa kuzingatia masharti ya vifungu vya 37 na 46 vya Sheria ya Uchaguzi tume inautaarifu Umma kuhusu ratiba ya uchaguzi wa jimbo hilo, kampeni za uchaguzi zitafanyika kati ya Aprili 29 hadi Mei 18, 2019 na siku ya uchaguzi itakuwa ni Mei 19”

Taarifa hii ya kufanyika kwa uchaguzi wa Jimbo la Arumeru inatokana na Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma kukubaliana na uamuzi wa Spika Ndugai kutangaza kuwa Joshua Nassari amepoteza sifa za kuwa Mbunge wa Jimbo hilo.

Nassari alivuliwa ubunge na Spika Ndugai Machi 14, 2019 kwa kilichodaiwa kuwa ni kutokana na kutohudhuria mikutano mitatu mfululizo bila taarifa rasmi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!