Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Takukuru waingia kazini ‘issue’ ya Nyalandu
Habari za Siasa

Takukuru waingia kazini ‘issue’ ya Nyalandu

Naibu Mkurugenzi wa Takukuru, Brigedia Jenerali
Spread the love

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), imesema kuwa suala la aliyekuwa Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu imelisikia na imeanza kulifanyia kazi, anaandika Angel Willium.

Takukuru wameingia kazini kulifanyia kazi shutuma za Nyalandu baada ya kutuhumiwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla, alipokuwa anachangia Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa mwaka 207/2018 na kuiagiza taasisi hiyo na polisi kumchunguza Nyalandu.

Naibu Mkurugenzi wa Takukuru, Brigedia Jenerali, John Mbungo amesema wamesikia tuhuma za Nyalandu na wameanza kuzichunguza na wakimkuta na hatia watamfikisha kunakostahili.

Mbugo ameitoa kauli hiyo leo ikiwa ni siku moja baada ya Waziri Dk. Kigwangala kumlipua Nyalandu akimtuhumu kwa matumizi mabaya ya madaraka.

Dk. Kigwangala amesema Nyalandu aliikosesha serikali mapato ya Sh. 32 bilioni kwa miaka miwili aliyohudumu katika wizara hiyo kwa kushindwa kusaini sheria ya tozo kwa hoteli za kitalii.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!