Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lijualikali arudi uraiani, Sumaye ampokea
Habari za SiasaTangulizi

Lijualikali arudi uraiani, Sumaye ampokea

Frederick Sumaye, Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Pwani (mwenye suti nyeusi) akiwa Peter Lijualikali, Mbunge wa Kilombero (suti ya kaki) na wanachama wa Chadema wakitoka gerezani Ukonga
Spread the love

FREDERICK Sumaye, Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Pwani, ameongoza viongozi wa Chadema waliofika kwenye gereza la Ukonga kumtoa Mbunge wa Kilombero, Peter Lijualikali, anaandika Pendo Omary.

Lijualikali ametoka gerezani baada ya kushinda rufaa yake jana katika Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam, baada ya kuhukumiwa kifungo cha miezo sita na mahakama ya Hakimu Mkazi Kilombero, Januari 11, 2017.

Sumaye alikuwa miongoni mwa vigogo wa Chadema ambao waliwasili gerezani hapo mapema leo asubuhi na kufuata taratibu za kumtoa mbunge huyo wa Kilombelo aliyekuwa anatumikia kifungo chake.

Viongozi hao wa Chadema wakiwa na mawakili wa Lijualikali waliofanikisha kushinda rufaa yake, walifanikiwa kumtoa mbunge huyo na kuendelea na shughuli nyingine.

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!