Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Shangwe zatawala mkutano mkuu Chadema
Habari za SiasaTangulizi

Shangwe zatawala mkutano mkuu Chadema

Spread the love

CHAMA Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kinafanya mkutano mkuu wake leo Jumanne tarehe 4 Agosti 2020 katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam. Anaripoti Brightness Boaz…(endelea)

Wajumbe wa mkutano huo wameanza kuingia ukumbini kuhudhuria mkutano huo utakaojadili masuala mbalimbali kikiwemo kuwathibitisha Tundu Lissu kuwa mgombe urais wa Tanzania, Salumu Mwalimu, mgombea mwenza.

Pia, mkutano huo, utathibitisha Said Issa Mohamed kuwa mgombea urais wa Zanzibar katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020.

Lissu alipendekezwa jana Jumatatu na wajumbe wa Baraza Kuu la Chadema kwa kura 405 kati ya 442 sawa na asilimia 91 huku Lazaro Nyalandu akipata kura 36 na Dk. Mayrose Majinge akiambulia kura moja.

Pia, mkutano huo mkuu utakaoongozwa na Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema, utaipitisha Ilani ya Uchaguzi Mkuu wa chama hicho.

Kinachoendelea kwa sasa ukumbini ni wajumbe kuendelea kuwasili na wengine kuserebuka mziki unaopigwa na bendi.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online, MwanaHALISI TV na mitandao yetu ya kijamii kwa habari na taarifa mbalimbali ya kinachoendelea

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!