Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali yawatangazia vita wanaotorosha madini
Habari za Siasa

Serikali yawatangazia vita wanaotorosha madini

Spread the love

SERIKALI imewatangazia vita watu wanaotorosha madini ya Tanzanite pamoja na wanaokwenda kinyume na matakwa ya sheria. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Akizungumza jana tarehe 01 Agosti, 2018 wakati alipofanya ziara ya kutembelea migodi ya madini ya Tanzanite na ukuta wa Mirerani mkoani Manyara, Waziri wa Madini, Angellah Kairuki aliwaonya wezi wa madini hayo kwamba kiama chao kinakuja.

Waziri Kairuki amesema serikali itaendelea kusimamia ulinzi na kudhibiti utoroshwaji wa madini hayo.

“Utoroshaji madini hausaidii, fedha ni za haraka lakini zinawaadhibu watanzania walio wengi kwa kuwa, fedha hizo hizo zingeweza kutumika katika miradi mingine ya maendeleo. Hivyo, kila mtanzania awe mlizi wa mwenzake,” amesema Kairuki.

Kwa upande wake,  Kamishna wa Madini, Mhandisi David Mlabwa, amesema  ni lazima Sheria, Kanuni na taratibu zizingatiwe wakati wa utekelezaji shughuli za uchimbaji madini kwa kuwa serikali inatambua mchango wa kila aina ya madini yanayopatikana nchini.

Naye, Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro, Tumaini Magesa ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Kiteto amesema kuwa, shughuli za uchimbaji katika eneo la Mirerani zinaendelea na hivyo serikali itaendelea kuboresha ulinzi na kuhakikisha kwamba unaimalika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!