Wednesday , 8 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli ateua wakili mkuu wa Serikali, Naibu wake
Habari za Siasa

Rais Magufuli ateua wakili mkuu wa Serikali, Naibu wake

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli amemteua Gabriel Pascal Malata kuwa Wakili Mkuu wa Serikali (Solicitor General). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Taarifa iliyotolewa leo Ijumaa tarehe 10 Julai,2020 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa imesema, kabla ya uteuzi huo, Malata alikuwa Naibu Wakili Mkuu wa Serikali na anachukua nafasi ya Dk. Julius Clement Mashamba.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amemteua Dk. Boniface Luhende kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Kabla ya uteuzi huo, Dk. Luhende alikuwa Mhadhiri katika Shule Kuu ya Sheria ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na anachukua nafasi ya Malata ambaye ameteuliwa kuwa Wakili Mkuu wa Serikali.

Msigwa amesema,uteuzi huo wa viongozi hao unaanza leo tarehe 10 Julai, 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

error: Content is protected !!