Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli aifungulia Qatar milango ya uwekezaji
Habari za Siasa

Rais Magufuli aifungulia Qatar milango ya uwekezaji

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS John Magufuli ameiomba nchi ya Qatar kushirikiana na serikali yake kwenye utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo, ikiwemo uzalishaji wa nishati ya umeme na ujenzi wa miundombinu. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Rais Magufuli ametoa ombi hilo leo tarehe 21 Machi 2019 wakati akizungumza na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar, Sheikh Mohammed bin Abdulrahman J.A Al Than, Ikulu jijini Dar es Salaam.

 Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa, inaeleza kwamba mazungumzo hayo ya Rais Magufuli na Sheikh Mohammed yalijikita katika namna ya kuboresha uhusiano wa mataifa hayo mawili hasa kwenye sekta ya gesi na madini.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa, Rais Magufuli alitangaza fursa za uwekezaji zilizopo nchini ikiwemo uchakataji wa gesi, madini, usafiri wa anga na utalii, na kumuomba Sheikh Mohammed kuwahamasisha wafanyabiashara wa Qatar kuja kuwekeza kwenye maeneo hayo.

“Natambua kuwa Qatar mna utaalamu wa kuchakata gesi na sisi tunayo gesi nyingi, kwa hivyo nawakaribisha mje tushirikiane kuwekeza katika sekta ya gesi na pia natambua kuwa nyie ni wanunuzi wakubwa wa dhahabu sisi tunayo dhahabu nyingi na hivi sasa tumeanzisha vituo vya ununuzi wa dhahabu. Nawakaribisha tutawapa ushirikiano wote mtaouhitaji,” amesema Rais Magufuli.

Naye Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi amesema baada ya Rais Magufuli na Sheikh Mohammed kuzungumza, atakunana na kiongozi huyo wa Qatar kwa ajili ya mazungumzo ya kina kuhusu maeneo ya ushirikiano.

Kwa upande wake Sheikh Mohammed, ameahidi kwamba Qatar itayafanyia kazi maombi ya Rais Magufuli ikiwemo kuzileta kampuni za nchi hiyo kuja kuwekeza katika maeneo yenye fursa zenye manufaa kwa pande zote mbili.

Mazungumzo hayo yalihudhuriwa na Balozi wa Tanzania nchini Qatar, Fatma Rajab na Balozi wa Qatar nchini Tanzania, Abdullah Jassim Mohammed Al Medadi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

Habari za Siasa

Wabunge waitaka TPDC kuongeza kasi ya kuunganisha wateja gesi asilia

Spread the love  KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini...

error: Content is protected !!