Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Prof. Shivji: Kuna sheria mbovu zinatungwa
Habari za Siasa

Prof. Shivji: Kuna sheria mbovu zinatungwa

Profesa Issa Shivji
Spread the love

MSOMI wa masuala ya sheria na utawala nchini Profesa Issa Shivji, ameeleza kukerwa na mwelekeo wa utungaji sheria mbovu kwa maslahi ya wachache. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Miongoni mwa mifano ya sheria mbovu alizotaja ni pamoja na Sheria ya Takwimu ya  mwaka 2018, inayomtaka mtu yoyote kutochapisha au kusambaza taarifa au chochote kuhusu takwimu mpaka apate kibali kutoka Ofisi ya  Taifa ya Takwimu (NBS).

Akizungumza katika kumbukizi ya miaka 16 ya kifo cha Jaji Francis Nyalali ilioandaliwa na taasisi ya Center for Strategic Litigation jijini Dar es Salaam leo tarehe 3 Aprili 2019 amesema, baadhi ya sheria zinatungwa kulenga watu ama kundi fulani.

“Hivi karibuni tumepitisha sheria nyingi mbovu, mfano hii Sheria ya Takwimu ambapo huwezi kufanya uchambuzi wowote wa kitakwimu na kuutoa mpaka upate kibali,” amesema.

Akimzungumzia Jaji Nyalali, Prof. Shivji amesema maisha yake yaenziwe kwa kuheshimu utawala wa sheria na kwamba, mchango wake (Jaji Nyalali) ulikuwa kwenye utawala wa sheria hivyo amelitaka taifa kusimama na urithi huo.

Jaji John Mroso amemuelezea Jaji Nyalali kwamba alikuwa anaumizwa anaposikia mahakama ikikosolewa, hasa kwenye  eneo la ucheleweshaji wa kesi.

“Wanasiasa walikuwa wakikosoa suala hilo ambapo ilimuumiza ikapelekea kusafiri kwenda nchini Marekani kwa ajili ya kupata uzoefu wa namna wanaendeshaje kesi,” amesema Jaji Mroso.

Jaji Mroso amesema, Jaji Nyalali ndiye aliyeanzisha mfumo wa kusimamia kesi za masikini bure. “Hakupendezwa na mtu yoyote aliyetaka kuingilia uhuru wa mahakama.”

Jaji Nyalali alihuduma kama Jaji Mkuu wa Tanzania kuanzia Mwaka 1977 hadi 2000 na kufariki terehe 2 Aprili 2003.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!