Tuesday , 30 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Pierre Liquid alamba dume
Habari za Siasa

Pierre Liquid alamba dume

Peter Mollel 'Piere Liquid' akisalimia wabunge alipopata mwaliko wa kutembelea bungeni
Spread the love

LICHA ya kuitwa mtu wa hovyo, mchekeshaji anayechipuka kwa kasi Peter Mollel ‘Pierre’ sasa ni lulu. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Kuitikia kwake mwaliko aliopewa wa kuwa mgeni maalum wa Mariamu Ditopile, Mbunge wa Viti Maalum (CCM) bungeni jijini Dodoma leo tarehe 3 Aprili 2019, kumeenda sambamba na ‘kulamba dume’ kutoka kwa Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa.

Pierre alikutana na Waziri Majaliwa ambaye alionesha kufurahishwa kwake kwa kukutana na mchekeshaji huyo.

Baada ya kupiga picha na Waziri Majaliwa, amemuahidi kumpa tiketi ya ndege kwa ajili ya kwenda kuishangilia Stars katika michuano ya Mataifa ya Afrika (AFCON) nchini Misri.

Wakati wa kutambulishwa kwake, Pierre ameshangiliwa na baadhi ya wabunge kuonesha umuhimu wake. Nderemo hizo zimefanyika licha ya kuitwa mtu wa hovyo wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Kuchangia Ujenzo wa Shule ya Wasichana Kisarawe, Pwani uliopewa jina la ‘Tokomeza Ziro’ mwishoni mwa wiki iliyopita.

Mara baada ya kumalizika kwa kipindi cha maswali na majibu, Spika Job Ndugai alimpa nafasi maalum Ditopile amtambulishe Pierre kwa kuwa yeye hamfahamu.

“Nina mgeni lakini simfahamu, naomba nimpe heshima Mheshimiwa Mariamu Ditopile atumie dakika moja kumtambulisha maana simfahamu,”amesema Spika Job Ndugai.

Akimtambulisha Pierre, Ditopile alisema ni Mtanzania (huku akisimama na kujipinda) mzalendo mjasiriamali wa fenicha anaepatikana Changombe. Ni mpenda burudani na ana kijiwe kinachoitwa Liquid.

“Lakini hivi karibuni ametokea kupata umaarufu wa hali ya juu, sio kwa nchi yetu hadi nje ya mipaka ya Tanzania kutokana na sanaa na vichekesho.

“Ndugu Pierre ni maarufu na kwa kauli zake ambazo huwafurahisha watu na hata kama una msongo wa mawazo, anauondoa.” amesema.

Hata hivyo, mbunge huyo ameeleza mchango wa Pierre katika kuleta hamasa kwa timu ya Taifa – Taifa Stars – kushinda bao 3 -0 dhidi ya Uganda.

“Ndugu Pierre karibu sana bungeni,” amesema Ndugai na kuongeza “Magufuli utabaki kuwa juu utabaki kileleni.”

Pia Pierre ameonekana kukonga nyoyo za baadhi ya wabunge ambapo baadhi yao pamoja na wafanyakazi wa Bunge kwa wakati tofauti, walipiga picha naye.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

Habari za Siasa

ACT Wazalendo yaanika madudu miradi ya ujenzi, moundombinu

Spread the loveCHAMA cha ACT Wazalendo kimeeleza wasiwasi juu ya uelekeo wa...

Habari za Siasa

Samia ashuhudia utiaji saini ujenzi wa minara 758 ya bilioni 265

Spread the love  RAIS Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa kampuni za...

error: Content is protected !!