JESHI la Polisi limezuia mkutano wa pamoja wa wabunge, Zitto Kabwe ( ACT), Upendo Peneza (Chadema) na John Heche (Chadema) wa kumnadi mgombea udiwani Chadema Kata ya Turwa wilayani Tarime. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Mkutano huo unadaiwa kuzuiwa kwa sababu ya Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi wa wilaya hiyo kusimamisha mikutano yote ya Chadema.
Zitto Kabwe ambaye pia ni Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo amesema Jeshi la Polisi linamshikilia Mbunge Esther Matiko pamoja na Mwandishi wa Habari wa Tanzania Daima, Tuma Sitta.
“Polisi wamenizuia kufika kituoni kumwona Mbunge Esther Matiko. Polisi wamevamia ofisi za Chadema Tarime na kurusha mabomu ya machozi. Udiwani tu unaleta maafa makubwa,” amesema Zitto.
Leave a comment