Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu aruhusiwa hospitalini, kutua nchini muda wowote
Habari za SiasaTangulizi

Lissu aruhusiwa hospitalini, kutua nchini muda wowote

Tundu Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki akiwa na mkewe nchini Ubelgiji akifanya mazoezi
Spread the love

TUNDU Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki ameruhusiwa kutoka hospitalini alipokuwa anatibiwa kwa miezi saba, nchini Ubelgiji. Anaripoti Mwandishi Weti … (endelea).

Lissu amesambaza ujumbe wake kupitia mitandao ya kijamii kuwa, ameruhusiwa kutoka hospitalini baada daktari wake kujiridhisha afya yake imetengamaa.

Mbunge huyo ameeleza katika ujumbe wake kuwa pamoja na kurusiwa lakini ataendelea kukaa na chuma pajani kwake kwa miezi saba.

Lissu katika ujumbe wake amemalizia kwa kuwaambia Watanzania, wanachokula wasimale kwani yupo karibu sana kurudi nchini.

Soma kamili ujumbe wa Lissu hapa chini

Hello Friends of Me!!!

Good afternoon to y’all. Kwa mara nyingine nawaleteeni habari njema.

Alfajiri ya tarehe 6 January ya mwaka huu, niliondoka Nairobi Hospital na kusafiri hadi Leuven, Ubelgiji, kwa ajili ya matibabu zaidi. Jana tarehe 6 Agosti ilikuwa mwezi wa saba kamili tangu niletwe hapa Ubelgiji kwa ajili hiyo.

Leo tarehe 7 Agosti ni miezi 11 to the day niliposhambuliwa na watu wanaojulikana sana kama ‘watu wasiojulikana.’

Tarehe 7 September mwaka jana sikulala nyumbani kwangu. Tarehe 7 Agosti ya leo, miezi 11 kamili baadae, nimeamkia nyumbani kwangu.

Tarehe 7 September iliyopita wote mlikuwa na hofu kubwa kama ningemaliza siku hiyo, au siku chache zilizofuata, nikiwa hai. Miezi 11 kamili baadae, Professor Dr. Wilhelmus Jan Mertsemakers, daktari wangu tangu nilipokuja University Hospital Leuven, amesema sina sababu ya kitabibu ya kuendelea kukaa hospitali.

Prof. Mertsemakers amesema nitaendelea na uponyaji nikiwa nyumbani kwangu. Nitatembelewa na homecare nurses kila siku nyumbani kuniangalia naendeleaje. Na nitarudi hospitali kumwona kila baada ya wiki mbili.

Bado nina lichuma kubwa kwenye paja liko kama antenna ya TV za mwaka ’47. Na Prof. Mertsemakers amesema nitakaa nalo kwa si chini ya miezi sita. Lakini habari ya mujini ndio hiyo: nimetoka hospitalini.

Hongereni sana kwa kazi nzuri ya kuniuguza na kuniponya. Na chochote mtakachokula au kunywa siku ya leo mnibakishie. Siko mbali.

Tundu Lissu,
Brussels, Belgium.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

error: Content is protected !!