Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi Dodoma wawashikilia ‘machangudoa’ 22
Habari Mchanganyiko

Polisi Dodoma wawashikilia ‘machangudoa’ 22

Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto
Spread the love

WANAWAKE takribani 22 pamoja na wanaume watano wanashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoa wa Dodoma kwa tuhuma za kujihusisha na biashara ya ngono. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza na wanahabari leo tarehe 9 Oktoba 2018 jijini Dodoma, Kamanda wa Polisi mkoani humo, Gilles Muroto amesema watuhumiwa hao walikamatwa maeneo ya Uhindini ambapo wanawake hao walikuwa wanauza miili yao wakati wanaume wawili walikuwa wateja wa baadhi ya wanawake hao.

Kamanda Muroto ameeleza kuwa, Jeshi la Polisi pia limekamata wamiliki wa baadhi ya baa zinazohifadhi ‘machangudoa’ hao.

“Tumekamata changudoa au dada poa hawa wanafanya umalaya, vile vile tumekamata baa zinazohifadhi watu hao maeneo ya Uhindini , tumekamata wamiliki wa baa na wanaume wawili. Wanaokimbilia akina dada,” amesema Kamanda Muroto.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Kengold wakabidhiwa kombe NBC Championship

Spread the loveMdhamini mkuu wa Ligi Daraja la Kwanza (NBC Championship) Benki...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

error: Content is protected !!