Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mwijage ajifananisha na Gaddafi
Habari za SiasaTangulizi

Mwijage ajifananisha na Gaddafi

Charles Mwijage, Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji. Picha ndogo Marehemu Muhammed Gaddafi
Spread the love

WAZIRI wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage amesema yeye ni muumini wa Mohammed Gaddafi, kwa kueleza kuwa yeye anafanya kazi ya kujenga mbali bila kujenga kwao na atajenga kwao mwishoni, anaandika Dany Tibason.

Licha ya Mwijage kuwa Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji pia ni mbunge wa Muleba Kaskazini, amesema yeye hawezi kujenga kwao kwanza na badala yake anaaza kujenga mbali na kwake kwa maana ya nyumbani kwake atajenga mwishoni wakati kaisha maliza sehemu nyingine.

Alitoa kauli hiyo leo bungeni alipokuwa akijibu swali la nyongeza la mbunge wa Viti Maalum, Sevelina Mwijage (CUF).

Sevelina katika swali lake la nyongeza alitaka kujua ni kwanini Waziri huyo ambaye anatokea katika mkoa wa Kagera ambaye ni mzawa wa Kagera na anaijua vizuri Kagera asianzishe kiwanda cha kuchakata mazao ya kahawa na chai ambalo ni zao linalolimwa mkoani humo.

“Waziri wewe ni mzaliwa wa mkoa wa Kagera ni kwanini usifikilie kuanzishwa kwa viwanda vya kuchakata zao la kahawa na majani ya chai ili wananchi kuondokana na umasikini,” amehoji Sevelina.

Awali katika swali la msingi la mbunge wa Ileje, Janet Mbene (CCM) alitaka kujua serikali ina mkakati gani wa kuanzisha viwanda vidogo ili kuongeza ajira kwa wananchi na kukupa pato la serikali.

Akijibu swali la nyongeza la mbunge wa Viti Maalum, Mwijage amesema kuwa yeye ni Muumini wa Muhammad Gaddafi kwani hawezi kujenga nyumbani kwanza anaanza na mbali anamalizia na nyumbani.

Pia amesema kwa sasa ameanzisha mazungumzo ya ujenzi wa kiwanda cha kuchakata maziwa ambacho kinaweza kufanya kazi vizuri.

Akijibu swali la msingi Mwijage amesema ili kutekeleza mikakati ya ujenzi wa viwanda, mamlaka za mikoa na wilaya zimeelekezwa kutenga maeneo mahususi kwa ajili ya kujenga viwanda vidogo vya kati na vikubwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

error: Content is protected !!