Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Musiba, Lugola waingia vitani
Habari za SiasaTangulizi

Musiba, Lugola waingia vitani

Spread the love

MUDA mchache baada ya Kangi Lugola, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi kumtaka Cyprian Musiba, anayejitambulisha kuwa mwanaharakati na mtetezi wa Rais John Magufuli kuacha upotoshaji, naye amemjibu ‘siachi.’ Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Musiba kwenye andiko lake katika ukurasa wake wa twitter leo tarehe 13 Sepemba 2019 amesema, haogopi kukamatwa na kwamba ataendelea.

Amesema, ni miaka mitatu sasa amekuwa akijitambulisha kama mwanaharakati lakini hakuwahi kusema ametumwa na serikali, CCM wala Ikulu.

“Lugola aache kutumia serikali kutaka kunidhibiti kwa sababu ni Waziri. Nimezaliwa siku moja, nitakufa siku moja na hizo jela wameumbiwa watu, kama anataka aje anikamate tu akaniweke. Anataka kuniziba mdomo kisa nimetoa msaada jimboni kwake, sitakubali,” ameandika Musiba.

Mapema leo tarehe 13 Septemba 2019, Lugola alizungumza na wanahabari na kutoa kauli ya onyo dhidi ya Musiba na kumtaka aache uzushi pia kuwadanganya wananchi kwamba uanaharakati wake una baraka za serikali.

Lugola alisema, Musiba amekuwa akichafua watu wakiwemo wanasiasa, wafanyabiashara na viongozi wa umma pamoja na kuwatia hofu.

Pamoja na andiko hilo, Musiba amedai kumshangaa Lugola kwa kuwa naye ni sehmu ya serikali ambayo yeye anaitetea na kuhoji, kwanini anataka kumfunga mdomo.

“Media zangu tunaandika vitu vizuri tu kuhusu serikali, yeye kama sehemu ya serikali sasa anataka kuniziba mdomo kisa nimetoa msaada jimboni kwake, sitakubali na hatoniziba mdomo, hawezi,” amesema Musiba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!