Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Uhifadhi magereza ni kwa mujibu wa sheria – Masauni
Habari za Siasa

Uhifadhi magereza ni kwa mujibu wa sheria – Masauni

Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamadi Masauni
Spread the love

SERIKALI imesema, moja ya jukumu la Jeshi la Magereza ni kuwapokea na kuwaifadhi waharifu wa aina zote, wanaopelekwa kwa mujibu wa sheria. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Kauli hiyo ilitolewa leo tarehe 13 Septemba 2019 bungeni na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni alipojibu swali na mbunge wa viti maalum, Nagma Giga (CCM).

Mbunge huyo alitaka kujua kama serikali haioni kuweka pamoja wafungwa na watuhumiwa ni hatari kwa mustakabali wa maisha yao ya baadaye.

Pia alitaka kujua, je serikali haioni imepoteza nguvu kazi ya vijana kwa kuwachanganya na wale wabakaji hususani vijana kuanzia miaka 18 hadi 30?

Akijibu swali hilo Masauni amesema, moja ya majukumu ya jeshi la magereza ni kuwapokea na kuwahifadhi magerezani wahalifu wa aina zote kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za nchi.

Amesema, sanjari na hilo kanuni za uendeshaji wa Magereza za mwaka 1967 zinaelekeza, uhifadhi wa waharifu utafanyika kwa kuzingatia utenganisho kwa vigezo vya jinsia, umri, kosa na Mifungo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!