Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Msanii Vitalis Maembe ajiunga ACT-Wazalendo, atangaza kugombea Bagamoyo
Habari za Siasa

Msanii Vitalis Maembe ajiunga ACT-Wazalendo, atangaza kugombea Bagamoyo

Spread the love

VITALIS Maembe, Mwanamuziki na Mwanaharakati nchini Tanzania, amesema amejiunga na Chama cha ACT-Wazalendo kwa kuwa chama hicho kina misingi ya  kudai haki  na kujipambanua kwenye ujamaa. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).

Maembe  amejiunga na chama hicho leo Jumatatu tarehe 29 Juni 2020 na kukabidhiwa kadi na Ado Shaibu, Katibu Mkuu wa chama hicho, makao makuu ya ACT-Wazalendo, Makumbusho jijini Dar es Salaam.

Maembe amesema ACT-Wazalendo ni chama chenye sifa anazozihitaji kama vile yeye anavyojipambanua kwenye muziki wake.

Amesema chama hicho kimejipambanua kwenye mapambano ya haki na kutetea wanyonge na kujenga umoja wa Afrika.

Kwa upande wake, Shaibu wakati anampokea Maembe amesema, mwanamziki huyo alijipambanua kwenye mtandao kuwa anahitaji kuendeleza mapambano ya haki kupitia siasa.

Wakati huo huo, Maembe amesema kuwa endapo chama hicho kitampa ridhaa atagombea ubunge Bagamoyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!