Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Moto wateketeza stoo shule ya Mivumoni Dar
Habari za Siasa

Moto wateketeza stoo shule ya Mivumoni Dar

Spread the love

SEHEMU ya Shule ya Mivumoni Islamic Seminary iliyoko ndani ya Msikiti wa Mtambani, Kinondoni jijini Dar es Salaam, imeteketea kwa moto, asubuhi ya leo Jumamosi tarehe 18 Julai 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Kwa mujibu wa Mariki Balongo, Mwalimu wa shule hiyo, moto huo ulianza majira ya saa 9:30 asubuhi, katika stoo ya shule hiyo.

Mwalimu huyo amesema, hakuna mwanafunzi aliyeathirika na tukio hilo, bali baadhi ya vifaa vya shule na vya wanafunzi viliteketea kwa moto.

Hata hivyo, Balongo amesema chanzo cha moto huo bado hakijajulikana.

“Ni kweli moto ulitokea sehemu ya stoo ya shule, ulianza saa tatu na nusu asubuhi. Hakuna mwanafunzi aliyedhurika lakini baadhi ya vifaa viliungua,” amesema Balongo.

Amesema moto huo ulidhibitiwa na kikosi cha zimamoto na uokoaji, kilichofika shuleni hapo saa 10:30 asubuhi.

“Chanzo cha moto hakijulikani nini hadi sasa. Na sidhani kama itakua umeme sababu kwenye hiyo stoo hakuna swichi zaidi ya taa ambayo swichi yake iko nje,” amesema Balongo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!