Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mil 160 zakatika kwenye uvuvi haramu
Habari Mchanganyiko

Mil 160 zakatika kwenye uvuvi haramu

Vyavu ambazo haziruhusiwi kuvulia zikiteketezwa kwa moto
Spread the love

MBUNGE wa Viti Maalum, Fakharia Shomari Khamis (CCM) ameihoji serikali namna ilivyojipanga katika kuzuia uvuvi haramu nchini, anaandika Dany Tibason.

Akiuliza swali bungeni leo, mbunge huyo pia ametaka kujua ni meli ngapi zilizokamatwa kwa sababu ya uvuvi haramu kuanzia mwaka 2010/15 lakini pia alitaka kujua ni watu wangapi wametiwa hatiani na hukumu zao zikoje.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, William Ole Nasha amesema katika kukabiliana na uvuvi haramu wizara imeanzisha na kuimarisha vituo 25 vya doria kwenye maziwa makubwa mwambao na Bahari ya Hindi na mipaka ya nchi.

Amesema vituo hivyo vipo katika maeneo ya Tanga, Dar es Salaam, Kigoma, Musoma, Kagera, Mwanza na Mtwara.

Vile vile amesema vituo vingine vipo Mafia, Kilwa, Horohoro, Kipili, Kasanga, Sota, Sitari, Kasumulo, Mbamba Bay Tunduma, Kanyigo, Rusumo, Ikola, Geita, Buhingu, Namanga na Murusagamba.

Amesema kuwepo kwa vituo hivyo kumeongeza uwezo wa kukabiliana na uvuvi na biashara haramu kupitia operesheni mbalimbali huku akisema kuwa pamoja na jitihada hizo za serikali tatizo la uvuvi haramu na biashara ya magendo kwenye mialo masoko na mipaka ya nchi bado ni kubwa.

Aidha amesema kuanzia mwaka 2011/15 jumla ya vyombo 2,795, injini za mitumbwi 118, magari 297 na pikipiki 33 vilikamatwa kwa sababu ya uvuvi haramu na utoroshwaji haramu kwenye maji hayo.

Amesema katika kipindi hicho jumla ya watuhumiwa 3,792 walikamatwa na kesi 243 zilifunguliwa mahakamani ambapo jumla ya Sh. 158,559,323 zilikusanywa ikiwa ni faini kutokana na makosa mbalimbali huku akisema katika kipindi hicho hakuna meli ya uvuvi iliyowahi kukamatwa.

Amewaomba wabunge ambao ni wajumbe katika halmashauri waendelee kutoa elimu kwa wavuvi kuhusu madhara ya uvuvi haramu na kuhimiza halmashauri zao kudhibiti uvuvi haramu kwenye maeneo yao.

Pia ameshauri jamii za wavuvi na wadau wote washirikishwe katika kusimamia rasilimali za uvuvi na matumizi endelevu kwa ajili ya kuwapatia wananchi ajira, chakula na u chumi wao na Taifa kwa ujumla kwa lengo la kudhibiti uvuvi haramu.

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Polisi wakanusha kufanya uzembe ajali iliyouwa mwandishi Ayo Tv

Spread the loveJESHI la Polisi limekanusha tuhuma zilizoibuliwa dhidi yake  kwamba limekawia...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

Habari Mchanganyiko

GGML yaja na teknolojia za kisasa maonesho ya OSHA Arusha

Spread the loveKATIKA kuelimisha wananchi na washiriki wa maonesho ya usalama na...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA wawanoa mama lishe 50 kukabiliana na majanga ya moto

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) kwa kushirikiana na...

error: Content is protected !!