Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mfumuko wa bei wapaa
Habari Mchanganyiko

Mfumuko wa bei wapaa

Spread the love

MFUMKO wa bei umeongezeka kutoka asilimia 3.2 mwezi Aprili, hadi asilimia 3.5 mwezi Mei mwaka huu. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa Irenius Ruyobwa, Mkurugenzi wa shughuli za kitakwimu Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) amesema, kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma kwa mwezi Mei imeongezeka ikilinganishwa na kasi iliyokuwepo Aprili mwaka huu.

Amesema, kuongezeka kwa mfumko huo kwa mwezi Mei, kumechangiwa na kuongezeka kwa bei za baadhi ya bidhaa za vyakula na bidhaa zisizo za vyakula kulinganisha na kipindi hiki mwaka 2018.

“Baadhi ya bidhaa za vyakula zilizochangia kuongezeka kwa mfumko wa bei kwa kipindi hicho ni pamoja na unga wa mahindi, nyama, samaki, matunda, viazi na mihogo mibichi,” alisema Ruyobwa.

Na kuwa, bidhaa zisizo za vyakula zilizochangia ongezeko la mfumko wa bei wa taifa ni mavazi, viatu, mkaa, vyombo vya jikoni, gharama za kumuona daktari hospitaliti za binafsi, dizeli na petroli.

Pia amesema, mfumko wa bei wa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa kipindi cha mwezi Mei, umeongezeka hadi asilimia 2.2 kutoka asilimia 0.9 kwa mwezi April 2019.

Kuhusu hali ya mfumko bei kwa nchi za Afrika Mashariki amesema, Uganda mfumko wa bei kwa mwisho wa mwezi Mei 2019 umepungua hadi asilimia 3.3 kutoka asilimia 3.5 kwa mwezi Aprili mwaka huu.

Kwa upande wa Kenya mfumuko wa bei kwa mwezi Mei, 2019 umepungua hadi asilimia 5.9 kutoka asilimia 6.58 kwa mwezi Aprili mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!