Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ‘Meya’ Isaya apata msoto Kisutu
Habari za Siasa

‘Meya’ Isaya apata msoto Kisutu

Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, imeahirisha kutoa uamuzi wa maombi ya Isaya Mwita, Meya wa Jiji la Dar es Salaam, kuzuia madiwani jijini humo, kufanya kkao cha kumuondoa madarakani. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).

Hii ni mara ya pili kwa mahakama hiyo kuahirisha kutoa uamuzi wa maombi ya Mwita, ambapo jana tarehe 8 Januari 2020, Hakimu Mkazi Kisutu, Janeth Mtega aliahirisha na kueleza angefanya hivyo leo tarehe 9 Januari 2020.

Maombi hayo yaliwasilishwa jana mahamani hapo, siku moja baada ya Sipora Liana, Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam kutoa wito wa kufanyika kikao hicho.

Kupitia wakili wake – Hekima Mwasipu – Isaya aliomba mahakama kuizuia kikao hicho kujadili ajenda ya kumuondolewa madarakani mpaka pale kesi ya msingi itakaposikilizwa.

Leo tarehe 9 Januari 2020, hakimu Mtega amesema, bado hajaandika uamizi, hivyo ataoa kesho saa tano asubuhi.

Wakati hakimu Mtega akisema hivyo, tayari kikao cha kumng’oa Isaya kimefanyika na kufikia hitimisho la kumuondoa madarakani licha ya akidi ya wajumbe kutokamilika.

Mahakamani hapo, wakili wa serikali Gabriel Malata, aliyewakilisha majabu, aliitaka mahakama kuyatupilia mbali maombi hayo.

Isaya amehudhuria mahakamani na gari aina ya Raum, ambayo si ile aliyokuwa akiitumia wakati akiwa meya. Gari ya umeya amenyang’anywa leo sambamba na ofisi yake kufungwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!