Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ‘Meya’ Isaya apata msoto Kisutu
Habari za Siasa

‘Meya’ Isaya apata msoto Kisutu

Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, imeahirisha kutoa uamuzi wa maombi ya Isaya Mwita, Meya wa Jiji la Dar es Salaam, kuzuia madiwani jijini humo, kufanya kkao cha kumuondoa madarakani. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).

Hii ni mara ya pili kwa mahakama hiyo kuahirisha kutoa uamuzi wa maombi ya Mwita, ambapo jana tarehe 8 Januari 2020, Hakimu Mkazi Kisutu, Janeth Mtega aliahirisha na kueleza angefanya hivyo leo tarehe 9 Januari 2020.

Maombi hayo yaliwasilishwa jana mahamani hapo, siku moja baada ya Sipora Liana, Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam kutoa wito wa kufanyika kikao hicho.

Kupitia wakili wake – Hekima Mwasipu – Isaya aliomba mahakama kuizuia kikao hicho kujadili ajenda ya kumuondolewa madarakani mpaka pale kesi ya msingi itakaposikilizwa.

Leo tarehe 9 Januari 2020, hakimu Mtega amesema, bado hajaandika uamizi, hivyo ataoa kesho saa tano asubuhi.

Wakati hakimu Mtega akisema hivyo, tayari kikao cha kumng’oa Isaya kimefanyika na kufikia hitimisho la kumuondoa madarakani licha ya akidi ya wajumbe kutokamilika.

Mahakamani hapo, wakili wa serikali Gabriel Malata, aliyewakilisha majabu, aliitaka mahakama kuyatupilia mbali maombi hayo.

Isaya amehudhuria mahakamani na gari aina ya Raum, ambayo si ile aliyokuwa akiitumia wakati akiwa meya. Gari ya umeya amenyang’anywa leo sambamba na ofisi yake kufungwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

error: Content is protected !!