MGOMBEA urais wa Tanzania kupitia chama cha upinzani ACT-Wazalendo, Bernard Kamillius Membe, amewakaribisha ndani ya chama hicho wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliokatwa kuwania ubunge. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Membe aliyewahi kuwa waziri wa mambo ya nje wa Tanzania kati ya mwaka 2007 hadi 2015 enzi za utawala wa awamu ya nne wa Rais mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete, ametoa ukaribisho huo jana Alhamisi tarehe 20 Agosti 2020.
Mwanadiplomasia huyo mashuhuri nchini aliyejiunga na ACT-Wazalendo tarehe 7 Julai 2020 baada ya kufukuzwa ndani ya chama alichokulia cha CCM amesema, waliokatwa ndani ya chama hicho kuwania kugombea ubunge wajiunge na ACT-Wazalendo.
Jana Alhamisi, CCM ilitangaza majina ya walioteuliwa kugombea ubunge katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020 huku ikishuhudia zaidi ya wabunge 70 wakishindwa kutetea nafasi zao.
https://twitter.com/BenMembe/status/1296562904431558658
Membe akitumia ukurasa wake wa Twitter ameandika “uteuzi wa CCM uliofanywa leo (jana) umenifurahisha sana! Nawapongeza wote waliobahatika kuteuliwa, lakini kubwa zaidi nawapa pole wale wote waliokatwa kwa sababu ya kuwa karibu nami.”
Soma zaidi:-
“Hiyo ni baraka siyo balaa. Karibuni mjiunge na ACT- Wazalendo haraka ili safari iendelee!” ameandika Membe ambaye ni Mshauri Mkuu wa ACT-Wazalendo.
Leave a comment