Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mchungaji Msigwa ajisalimisha Oysterbay
Habari za Siasa

Mchungaji Msigwa ajisalimisha Oysterbay

Mch. Peter Msigwa, Mbunge wa Iringa Mjini
Spread the love

MCHUNGAJI Peter Msigwa, Mbunge wa Iringa Mjini yuko njiani kujisalimisha katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay, jijini Dar es Salaam. Ni baada ya mahakama kuagiza akamatwe. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).                

Msigwa ametoa taarifa hiyo leo tarehe 18 Novemba 2019, kupitia ukurasa wake wa Twitter, siku tatu baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuagiza wabunge wanne wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kukamatwa, kwa kushindwa kufika mahakamani hapo.    

Mbunge huyo wa Iringa Mjini amesema, amepigiwa simu na Jeshi la Polisi, kumtaarifu kwamba anatakiwa kuripoti katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay.

“Nimepigiwa simu na Jeshi la Polisi, natakiwa kuripoti kituo cha polisi cha Oysterbay Dar, niko njiani kuelekea huko,” ameandika Msigwa.

Msigwa anakuwa mbunge wa pili wa Chadema kujisalimisha kituoni hapo, baada ya Halima Mdee, Mbunge wa Kawe, kujisalimisha kituoni hapo siku ya Jumamosi iliyopita.

Wabunge wengine wanaotakiwa kujisalimisha polisi kwa amri ya mahakama ni Ester Bulaya (Bunda Mjini) na John Heche (Mbunge wa Tarime Mijijini).

Umuzi wa kukamatwa wabunge hao ulitolewa leo tarehe 15 Novemba 2019 na Hakimu Mkuu Mkazi wa mahakama hiyo, Thomas Simba kutokana na wabunge hao kushindwa kufika mahakamani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!