MCHUNGAJI Peter Msigwa, Mbunge wa Iringa Mjini yuko njiani kujisalimisha katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay, jijini Dar es Salaam. Ni baada ya mahakama kuagiza akamatwe. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).
Msigwa ametoa taarifa hiyo leo tarehe 18 Novemba 2019, kupitia ukurasa wake wa Twitter, siku tatu baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuagiza wabunge wanne wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kukamatwa, kwa kushindwa kufika mahakamani hapo.
Mbunge huyo wa Iringa Mjini amesema, amepigiwa simu na Jeshi la Polisi, kumtaarifu kwamba anatakiwa kuripoti katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay.
“Nimepigiwa simu na Jeshi la Polisi, natakiwa kuripoti kituo cha polisi cha Oysterbay Dar, niko njiani kuelekea huko,” ameandika Msigwa.
Nimepigiwa simu na Jeshi la Polisi , natakiwa kuriport kituo cha polisi Osterbey Dar. Niko njiani kuelekea huko .
— peter msigwa (@MsigwaPeter) November 18, 2019
Msigwa anakuwa mbunge wa pili wa Chadema kujisalimisha kituoni hapo, baada ya Halima Mdee, Mbunge wa Kawe, kujisalimisha kituoni hapo siku ya Jumamosi iliyopita.
Wabunge wengine wanaotakiwa kujisalimisha polisi kwa amri ya mahakama ni Ester Bulaya (Bunda Mjini) na John Heche (Mbunge wa Tarime Mijijini).
Umuzi wa kukamatwa wabunge hao ulitolewa leo tarehe 15 Novemba 2019 na Hakimu Mkuu Mkazi wa mahakama hiyo, Thomas Simba kutokana na wabunge hao kushindwa kufika mahakamani.
Leave a comment