Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mchungaji Msigwa ajisalimisha Oysterbay
Habari za Siasa

Mchungaji Msigwa ajisalimisha Oysterbay

Mch. Peter Msigwa, Mbunge wa Iringa Mjini
Spread the love

MCHUNGAJI Peter Msigwa, Mbunge wa Iringa Mjini yuko njiani kujisalimisha katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay, jijini Dar es Salaam. Ni baada ya mahakama kuagiza akamatwe. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).                

Msigwa ametoa taarifa hiyo leo tarehe 18 Novemba 2019, kupitia ukurasa wake wa Twitter, siku tatu baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuagiza wabunge wanne wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kukamatwa, kwa kushindwa kufika mahakamani hapo.    

Mbunge huyo wa Iringa Mjini amesema, amepigiwa simu na Jeshi la Polisi, kumtaarifu kwamba anatakiwa kuripoti katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay.

“Nimepigiwa simu na Jeshi la Polisi, natakiwa kuripoti kituo cha polisi cha Oysterbay Dar, niko njiani kuelekea huko,” ameandika Msigwa.

Msigwa anakuwa mbunge wa pili wa Chadema kujisalimisha kituoni hapo, baada ya Halima Mdee, Mbunge wa Kawe, kujisalimisha kituoni hapo siku ya Jumamosi iliyopita.

Wabunge wengine wanaotakiwa kujisalimisha polisi kwa amri ya mahakama ni Ester Bulaya (Bunda Mjini) na John Heche (Mbunge wa Tarime Mijijini).

Umuzi wa kukamatwa wabunge hao ulitolewa leo tarehe 15 Novemba 2019 na Hakimu Mkuu Mkazi wa mahakama hiyo, Thomas Simba kutokana na wabunge hao kushindwa kufika mahakamani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!