Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge Mtulia chali Kinondoni, Tarimba apeta
Habari za SiasaTangulizi

Mbunge Mtulia chali Kinondoni, Tarimba apeta

Maulid Mtulia
Spread the love

MAULID Mtulia, Mbunge anayemaliza muda wake jimbo la Kinondoni jijini Dar es Salaam, ameshindwa kutetea nafasi yake katika kura za maoni za Chama Cha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea)

Mtulia ameangushwa na Abbas Tarimba katika kura hizo za maoni zilizofanyika leo Jumatatu tarehe 20 Julai 2020 katika Ukumbi wa King Solomon.

Wagombea walikuwa 79 ambapo Tarimba amepata kura 171, mbunge wa zamani wa jimbo hilo, Iddi Azzan kura 77 na Mtulia kura 11 kati ya kura zote 404 zilizopigwa na wajumbe wote.

Wagombea wengine wamekukuta wakipata sifuri, kura moja, tatu au nne.
Matokeo hayo yametangazwa na Frank Kamugisha, msimamizi wa uchaguzi na mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi wa CCM mkoa wa Dar es Salaam.

        Soma zaidi:

https://www.youtube.com/watch?v=HrgzMOSHohw

Katika uchaguzi mkuu wa tarehe 25 Oktoba 2015, Mtulia alishinda akiwa Chama Cha Wananchi (CUF) lakini tarehe 2 Desemba 2017 alitangaza kujizulu nafasi hiyo na kuhamia CCM kuunga juhudi zinazofanywa na Serikali chini ya Rais John Magufuli.

Uchaguzi uliporudiwa, CCM ilimpitisha tena Mtulia kuwania nafasi hiyohiyo na kuibuka mshindi tena akimshinda Salum Mwalimu wa Chadema.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!