Tuesday , 5 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Polisi wamwacha Sheikh Ponda kwa dhamana
Habari Mchanganyiko

Polisi wamwacha Sheikh Ponda kwa dhamana

Sheikh Issa Ponda Issa, Katibu wa Jumuiya ya Taasisi za Kiislam Tanzania akiwa mahakamani katika moja ya kesi zake
Spread the love

SHEIKH Ponda Issa Ponda, Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislam nchini, ameachwa na Jeshi la Polisi kwa dhamana. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Akizungumza na MwanaHALISI Online, Ibrahim Mkondo ambaye ni Katibu wa Sheikh Ponda amesema, Sheikh Ponda ameachwa leo tarehe 20 Julai 2020, mchana.

“Sheikh ametoka leo, ameambiwa kesho saa 2 anatakiwa kuripoti polisi,” amesema Mkondo.

Sheikh Ponda alikamatwa tarehe 11 Julai 2020, alipokuwa ofisini kwake katika Msikiti wa Bungoni, jijini Dar es Salaam kwa madai ya kuandika waraka wenye uchochezi.

Kwenye waraka huo uliosomwa na Sheikh Ponda Issa Ponda, tarehe 9 Julai 2020 jijini Dar es Salaam, miongoni mwa mambo yaliyomo kwenye waraka huo ni pamoja na kuitaka serikali kuhakikisha uchaguzi mkuu wa mwaka huu unakuwa huru na haki, pia umuhimu wa kuwa na Katiba Mpya.

“Kwa hakika maelezo yetu ya nini tunataka kwa taifa letu katika uchaguzi huu, yangekuwa na maana sana kama Taifa lingekuwa na Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Tume Huru ya Uchaguzi, vinavyotokana na Wananchi wenyewe,” alisema Sheikh Ponda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

RPC Songwe awafunda trafki kuzingatia uadilifu

Spread the loveASKARI wa kikosi cha usalama barabarani mkoani Songwe wametakiwa kuendelea...

Habari Mchanganyiko

Mchimba madini jela maisha kwa kubaka, alihonga Sh 500

Spread the loveMahakama ya wilaya ya Songwe imemtia hatiani na kumhukumu kifungo...

Habari Mchanganyiko

Mlima wa Moto wazindua kongamano la SHILO kumuenzi Rwakatare

Spread the loveKANISA la Mlima wa Moto Mikocheni jijini Dar es Salaam,...

Habari MchanganyikoTangulizi

20 wafariki dunia kwa mafuriko Manyara

Spread the loveMVUA za vuli zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini zimeleta madhara...

error: Content is protected !!