Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe bado mgonjwa, aomba kughairishwa kesi yeke
Habari za Siasa

Mbowe bado mgonjwa, aomba kughairishwa kesi yeke

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

FREEMAN Mbowe, mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ameiomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kupumzika kutokana na hali ya afya yake kutoimarika. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Mbowe na wenzake wanane wanashtakiwa kwenye mahakama hiyo kwa mashitaka 13 yakiwemo kufanya kusanyiko kinyume cha sheria, kutoa maneno ya uchechezi na kusababishia kifo Akwiline Akwilina, mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa Chuo cha Usafirishaji cha taifa (NIT).

Washtakiwa wengine katika kesi hiyo, ni Dk. Vecent Mashinji, katibu mkuu wa chama hicho; John Mnyika, naibu katibu mkuu (Bara); Salum Mwalim, naibu katibu mkuu Zanzibar na Halima James Mdee, mbunge wa Kawe na mwenyeti wa Baraza la Wanawake la chama hicho (BAWACHA).

Wengine waliomo kwenye kesi hiyo, Na. 112 ya mwaka 2018, ni Ester Matiko, mbunge wa Tarime Mjini;

Peter Msigwa, mbunge wa Iringa Mjini, John Heche, mbunge wa Tarime Vijijini na Ester Bulaya, mbunge wa Bunda Mjini.

Akiwasilisha maombi ya kutoendelea kwa kesi hiyo, wakili wa Mbowe, Jeremiah Mtobesya, alimueleza Hakimu Mkazi Mkuu wa mahakama hiyo, Thomas Simba, kwamba Mbowe alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa Homa ya Dengue, Malaria na shinikizo la damu na kwamba ameruhusiwa kutoka hospitali siku ya Ijumaa tarehe 22 Novemba 2019.

Amesema, pamoja na kutoka hospitali, hali ya mwanasiasa huyo wa upinzani, bado haijatengemaa. Akaomba  kuarishwa kwa shauri hilo ilia pate muda wa kupumzika.

Hata hivyo, upande wa mashitaka unaoongozwa na Wakili Mkuu wa Serikali, Faraja Nchimbi, umepinga maombi hayo.

Nchimbi amedai, afya ya Mbowe imekaa sawa na kwa kuwa shauri hilo limekuwa likikwama kwa sababu kama hizo, ameiomba mahakama kuendelea kusikiliza shauri hilo.

Baada ya kusikiliza pande zote mbili, Hakimu Simba amedai, suala la afya ni muhimu kwa kila binadamu na hivyo anaaihirisha sahuri hilo, hadi tarehe 28 Novemba 2019.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!