Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Masogange ana kesi ya kujibu Kisutu
Habari Mchanganyiko

Masogange ana kesi ya kujibu Kisutu

Agnes Masogange akiwasili mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu
Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imesema msanii wa filamu nchini, Aggnes Masogange ana kesi ya kujibu kwenye mashtaka yake ya matumizi ya dawa za kulevya, anaandika Faki Sosi.

Leo Hakimu Mkazi Wilbard Mashauri ametoa uamuzi huo baada ya upande wa Jamhuri kumaliza kuwasilisha ushahidi wake mahakamani hapo.

Ushahidi huo ulitolewa na askari wa Jeshi la Polisi, Sospiter kutoka ofisi ya upelelezi ya kituo kikuu cha Polisi kanda Maalumu ya Dar es Salaam.

Sospiter alidai mahakamani hapo kuwa baada ya kumpekuwa mtuhumiwa Masogonge alimkabidhi askari wa kike (WP), Judicy na kwenda naye kwa mkemia kwa ajili ya kupimwa mkojo.

Hakimu Mashauri alimuuliza mtuhumiwa baada ya kumkuta na hatia kwamba ni kwa namna gani atajitetea mahakamani hapo kati ya njia tatu ya kuwasilisha kiapo, kuleta mashahidi au kukaa kimya.

Mtuhumiwa Masogange aliomba kuleta kiapo na kuleta mashahidi watatu mahakamani hapo.
Kesi hiyo itatajwa tena Oktoba 12 mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!