Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Lisu kupamba tamasha la injili
Habari MchanganyikoTangulizi

Lisu kupamba tamasha la injili

Tundu Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki
Spread the love

MWIMBAJI wa nyimbo za injili, John Lisu anatarajia kutikisa katika tamasha la uamsho lililoanza ambalo litashirikisha watui wote bila kujali itikadi za dini zao, anaandika Dany Tibason.

Katika mahojiano maalumu na gazeti hili Mchungaji kiongozi wa Kanisa la Tanzania Assemblies Of God (victory Christian center) DK. Huruma Nkone alisema wameandaa mkutano wa uamsho unaoshirikisha watu wote bila kujali utofauti wa madhehebu.

Akifafananua zaidi amesema mhubiri katika mkutano huo wa uamsho ni Askofu Yona Suleiman kutoka kiomboi mkoani Singida.

Tamasha hilo la uamsho litafanyika katika ukumbi wa Kanisa la Victory Christian Center na utafanyika jijini Dar es Salaam.

Amesema wakazi wa jiji la Dar es Salaam wanakabiribishwa ili kusikia neno la Mungu ambalo litatolewa na wahubiri mbalimbali.

“Ni kwa neema na waimbaji wengine watapamba mkutano huo wa uamsho ni Rivers of Joy International Kwaya ya Kanisa la KLPT Tageta na nyingine nyingi”alieleza Dk.Nkone.

DK Nkone ametoa wito kwa wakazi wa jiji la Dar kujitokeza kwa wingi kwani huduma ya maombi na maombezi itatolewa bure.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

error: Content is protected !!