Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Madini kibao yagundulika Ukanda wa Pwani
Habari Mchanganyiko

Madini kibao yagundulika Ukanda wa Pwani

Aina mbalimbali za madini yanayopatikana Ukanda wa Pwani
Spread the love

SERIKALI imekiri kwamba kwenye Ukanda wa Pwani ya Tanzania kunapatikana madini ya aina mbalimbali ambayo ni barite, chokaa, chumvi, clay, dhahabu, flourite, jasi, kaolin, mchanga, mercury, niobim, ruby, rutile, titanium, zircon na gesi asilia, anaandika Dany Tibason.

Hayo yalielezwa leo bungeni na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk. Medad Kaleman alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Rufiji, Mohammed Mchengerwa (CCM) ambalo liliulizwa kwa niaba yake na Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega (CCM).

Ulega alihoji kuhusina na maeneo mengi ya Pwani huwa na madini mengi, Je, eneo la Rufiji lina madini mengi ili wananchi hao washauriwe ipasavyo kutouza maeneo hayo.

Akijibu, Dk. Kalemani alisema ni kweli kwamba kwenye ukanda wa Pwani wa Tanzania kunapatikana madini ya aina mbalimbali ambayo ni pamoja na barite, chokaa, chumvi, clay, dhahabu, flourite, jasi, kaolin, mchanga, mercury, niobim, ruby, rutile, titanium, zircon na gesi asilia.

Amesema wakala wa Jiolojia Tanzania (GST) kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Kampuni ya Beak Consultants GmbH ya nchini Ujerumani ilifanya utafiti wa awali  kati ya mwaka 2013 na 2014.

‘’Kutokana na utafiti huo madini yaliyobainika katika eneo la Rufiji ni pamoja na chokaa na niobium ambayo hupatikana katika eneo la Luhombero.

Pia alidai kuna viashiria  vya uwepo wa Madini ya barite, dhahabu, flourite, mercury na sulfur katika maeneo ya Wingayongo karibu na Kibiti.

‘’Utafiti wa kina unahitajika ili kubaini kiasi halisi cha mashapo ya madini yaliyopo katika maeneo hayo,’’ amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!