Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Machozi yenu yataniumiza – Rais Magufuli
Habari za Siasa

Machozi yenu yataniumiza – Rais Magufuli

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS John Magufuli amesema hawezi kuongoza nchi iliyotawaliwa na machozi pamoja na watu wanaosikitika kwa unyonge. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma leo tarehe 17 Julai 2019.

Akizungumza na wananchi hao, Rais Magufuli amesema machozi ya wananchi yatamuumiza.

“Siwezi nikatawala nchi ya machozi, machozi haya yataniumiza. Siwezi nikatawala watu wanaosikitika wako kwenye unyonge na unyonge wao uko kwenye kuonwa,” amesema Rais Magufuli.

Aidha, Rais Magufuli amezungumzia hatua ya Biswalo Mganga, Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), kuwafutia kesi uhujumu uchumi, polisi nane waliotuhumiwa kutorosha shehena ya dhahabu.

“Hata wale polisi walioshikwa kwa wizi wa dhahabu waliokuwa wanasindikiza kule Mwanza, hata kwa kuwaona tu unaweza ukajua kwenye macho yao. DPP naye amewaachia na mimi niliamua warudishwe kazini sababu walikuwa wameshafukuzwa,” amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli amesema tukio hilo liwe fundishi kwa polisi wanaopenda kujihusisha na vitendo vya rushwa.

Wakati huo huo, Rais Magufuli ameagiza Wizara ya Katiba na Sheria pamoja na vyombo vya ulinzi na usalama kuwaacha huru wafungwa wasiohitajika kuwepo gerezani.

 “Nilishatoa maelekezo kwa Wizara ya Katiba na Sheria pamoja na vyombo vingine vya ulinzi na usalama, wapitie Magereza yote wazungumze na watuhumiwa walio mahabusu ili wale ambao hawahitajiki kukaa mule waachiwe,” amesema JPM.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!