Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Lukuvi atangaza kubadilisha hati za ardhi 2018
Habari Mchanganyiko

Lukuvi atangaza kubadilisha hati za ardhi 2018

William Lukuvi, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi
Spread the love

WAZIRI wa Ardhi ,Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amemtaka Mkurugenzi wa Tehama katika wizara hiyo, ifikapo 2018, mradi wa mfumo unganishi wa taarifa za ardhi katika mtandao uwe umekamilika, anaandika Angel Willium.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Lukuvi amesema amesema ifikapo mwakani inatakiwa kuzinduliwa na kuanza kazi.

“Mkurugenzi hakuniambia ni tarehe ngapi kazi itakamilika, hivyo ifikapo mwakani tarehe moja mwezi wa sita, mfumo huu utazinduliwa na uanze kufanya kazi, hati mpya itaanza kutolewa na wale wenye hati za zamani watabadilishiwa amesema Lukuvi.

Aidha, Mkurugenzi wa Tehama wa wizara hiyo, Shaban Pazi amesema mfumo unganishi wa kutunza taarifa katika mtandao, kwa sasa ndiyo wanauandaa na wataanza na mkoa wa Dar es Salaam katika wilaya ya Kinondoni na Ubungo na kufatia mikoa yote ya Tanzania.

Pazi amesema lengo la mradi ni kuimarisha usalama katika umiliki wa ardhi, kutoa huduma nafuu na sahihi kwa wateja, kupunguza muda wa kuhakiki na kuhamisha ardhi, kuzuia uvamizi wa misitu, hifadhi za barabara na sehemu zilizokuwa wazi na kupunguza rushwa katika malipo.

Mradi huo ulianza mwezi Julai 2016 na unadhaminiwa na benki ya Dunia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!