Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lowassa, Sumaye, Maalim Seif, Zitto kumfuata Mbowe Kisutu kesho
Habari za SiasaTangulizi

Lowassa, Sumaye, Maalim Seif, Zitto kumfuata Mbowe Kisutu kesho

Spread the love

VIGOGO watatu wa kisiasa nchini, Edward Lowassa, Maalim Seif Sharif Hamad na Fredrick Suamye, kesho Ijumaa, wataongoza mamia ya wafuasi wa upinzani, kuelekea kwenye Mahakama ya Kisutu, jijini Dar es Salaam, kufuatilia kesi ya “kisiasa,” inayomkabili mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe. Anaripoti Saed Kubenea … (endelea).

Wengine watakaongozana na viongozi hao, ni Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo) ambaye pia ni kiongozi mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe, wabunge wa upinzani na baadhi ya viongozi wa vyama vingine.

Mbowe yuko kwenye mahabusu ya magareza ya Segerea, baada ya kufutiwa dhamana na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, tokea Novemba mwaka huu.

Mwingine ambaye yuko mahabusu ya Segerea baada ya kufutiwa dhamana na Mahakama ni mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko.

“Kesho tarehe 21 Desemba 2018, saa mbili asubuhi, kwenye Mahakama ya Hakim Mkazi Kisutu, wafungwa wa kisiasa (Freeman Mbowe na Esther Matiko), wataletwa mahakamani kwa ajili ya kutajwa kesi yao, wakati wakisubiri kuitwa mahakama ya rufaa,” imeeleza taarifa ya viongozi hao.

Imesema, “Maalim Seif, Lowassa, Sumaye na Zitto, wamethibitisha kuongoza mamia ya wananchi kuhudhuria mahakamani. Shime kwa wapigania demokrasia, haki na utu, kujitokeza kwa wingi kuwalaki wafungwa hawa wa kisiasa.”

Washitakiwa wengine kwenye kesi hiyo, ni Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Vicenti Mashinji; naibu katibu mkuu wa chama hicho Zanzibar, Salum Mwalimu na mbunge wa Kawe, Halima Mdee.

Wengine, ni Naibu katibu Mkuu Bara na mbunge wa Kibamba, John Mnyika, Ester Bulaya, mbunge wa Bunda, Mchungaji Peter Msigwa, mbunge wa Iringa Mjini na John Heche, mbunge wa Tarime Vijijini.

Mbowe na wenzake, wanashitakiwa mahakamani kwa madai ya kuandamana bila kibali na kusababisha mauwaji ya mwanafunzi wa chuo cha usafirishaji cha taifa (NIT), Akwiline Akwilina.

Akwilina aliuawa kwa kupigwa risasi na polisi, Februari mwaka huu, katika maeneo ya Mkwajuni jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo Polisi waliokuwa wakishikiliwa kwa tuhuma za mauaji hayo, waliachiwa huru kwa madai kuwa hakukuwa na ushahidi juu ya tuhuma hizo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!