TUNDU Lissu, mgombea urais wa Tanzania kupitia Chadema ametembelea Mlimani City jijini Dar es Salaam na kufanya manunuzi mbalimbali katika moja ya maduka. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Lissu anaendelea kutumikia adhabu ya kufungiwa siku saba kutokufanya kampeni kwa siku saba na Kamati ya Kitaifa ya Maadili ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuanzia tarehe 3 Oktoba 2020, itahitimishwa kesho Ijumaa.
Jana Jumatano, Lissu alitembelea maeneo mbalimbali ya Kariakoo jijini humo na kufanya manunuzi mbalimbali ikiwemo mchele na matunda.
Leo Alhamisi mchana tarehe 8 Oktoba 2020, Lissu ameonekana katika madaku ya Mlimani City akinunua bidhaa mbalimbali na baadaye anatarajiwa kwenda soko la Manzese ambako nako atanunua bidhaa akiwa huko.
Leave a comment