Thursday , 7 December 2023
Home Kitengo Michezo Bocco awekwa nje kikosi cha Taifa Stars
Michezo

Bocco awekwa nje kikosi cha Taifa Stars

Spread the love

KOCHA wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ Etiene Ndayilagije amemuweka nje ya kikosi mshambuliaji wa klabu ya Simba John Bocco kutokana na kusumbuliwa na majeruhi na hivyo kumpa muda kwa ajili ya matibabu. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mazoezi hayo ambayo yameendelea leo kwenye viwanja vya Gymkhana Jijini Dar es Salaam kwa siku ya pili toka kikosi hicho kilivyoingia kambini siku ya Jumatatu.

Kabla ya mazoezi hayo Ndayilagije alielezea hali ya kikosi chake baada ya mazoezi ya siku mbili, huku akitoa sababu ya nahodha wa klabu ya Simba, John Bocco kutokuwepo kwenye kikosi hiko.

“Tatizo kidogo lilitokea kwa Bocco ambaye hakuwa vizuri tumeona aendelee na matibabu kwa kuwa tumeona hawezi kuendelea, lakini wachezaji wote wamefika kasoro Himidi Mao ambaye ataingia baadae lakini wote wana hali nzuri,” alisema kocha huyo.

Etiene Ndayilagije, kocha wa timu ya Taifa Stars

Stars inatarajia kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Burundi siku ya Jumapili 11 Oktoba, 2020 kwenye Uwanja wa Benjamini Mkapa majira ya saa 10 jioni katika kujiweka sawa na mchezo wa kufuzu Afcon dhidi ya Tunisia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Piga mkwanja wa kutosha katika usiku wa kibabe kati ya Man United vs Chelsea

Spread the love USIKU wa leo katika dimba la Old Trafford utapigwa mchezowa...

BiasharaMichezo

Mwana FA anogesha Tamasha la Exim Bima Festival

Spread the loveNAIBU Waziri Wa Utamaduni, Sanaa Na Michezo, Hamis Mwinjuma ‘Mwana...

Michezo

Manchester City dhidi ya Tottenham ni usiku wa kisasi

Spread the love KIPUTE kati ya klabu ya Manchester City dhidi yaTottenham Hotspurs...

Michezo

Wikiendi ya kutamba na Meridianbet hii hapa usikubali kuikosa

Spread the loveMERIDIANBET wanakwenda kukupa nafasi ya kutambawikiendi hii kupitia ODDS KUBWA walizoweka...

error: Content is protected !!