Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea: Siondoki Chadema, nitagombea tena Ubungo
Habari za SiasaTangulizi

Kubenea: Siondoki Chadema, nitagombea tena Ubungo

Saed Kubenea, Mbunge wa Ubungo
Spread the love

SAED Kubenea, Mbunge wa Ubungo kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), amesema atagombea tena jimbo hilo kupitia chama hicho, katika Uchaguzi Mkuu Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kubenea ametangaza uamuzi huo leo Jumamosi tarehe 13 Juni 2020 jijini Dar es Salaam, katika mkutano wake uliolenga kueleza aliyoyafanya katika kipindi cha miaka mitano kwa  wadau wa jimbo la Ubungo.

Kubenea amesema muda wa uchukuaji fomu katika chama chake ukifika, atajitokeza katika kinyang’anyiro hicho.

Kubenea amesema, anaamini Kamati Kuu ya Chadema itampitisha tena kugombea jimbo hilo huku akisisitiza, hana mpango wa kuondoka katika chama hicho.

“Muda ukifika wa uchukuaji fomu katika Jimbo la Ubungo, nami nakusudia kuchukua na kugombea tena. Naomba mpuuze kauli za mitaani,” amesema Kubenea.

“Mimi niko Chadema, siondoki Chadema, nitagombea ubunge na naamini Kamati Kuu ya Chadema itanipitisha kwa sababu zilezile ilizotumia katika uchaguzi uliopita,” amesema Kubenea huku akishangiliwa na wadau waliojitokeza kumsikiliza.

Kauli hiyo ya msisitizo ya Kubenea kuhusu kutohama Chadema, imekuja kufuata tuhuma kadhaa kutoka kwa baadhi ya watu kwamba anataka kuondoka kwenye chama hicho na kugombea Ubunge kupitia chama kingine.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!