Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea, Komu wapewa onyo kali, wawekwa chini ya uangalizi
Habari za SiasaTangulizi

Kubenea, Komu wapewa onyo kali, wawekwa chini ya uangalizi

Spread the love

KAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimewapa onyo kali wabunge wake Saed Kubenea wa Ubungo na Anthony Komu wa Moshi Vijijini kufuatia kuwatia hatiani juu ya kuunda njama ovu dhidi ya Mwenyekiti Freeman Mbowe na Meya wa Ubungo, Boniface Jacob. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika amesema Kamati Kuu imewatia hatiani wabunge hao baada ya kuwatia mbele ya kamati hiyo kujieleza na wote wamekiri kuwa sauti iliyosambaa ni yao wameomba radhi.

Mnyika amesema baada ya wabunge hao kukiri na kuomba radhi, kamati imefanya maamuzi juu ya makosa yao, kwanza kuwapa onyo kali, pili waandike barua ya kuomba radhi kwa chama.

Pia Mnyika amesema kamati kuu ikafikia uamuzi wa kuwaweka kwenye uangalizi kwa miezi 12, ikiwa oamoja na kuwavua nafasi zao zote za uongozi ndani ya chama na kubaki na ubunge.

Naibu Katibu amesema adhabu ya mwisho kwa wabunge hao ni kutoka hadharani kuomba radhi kwa makosa waliyofanya dhidi ya viongozi wa chama hicho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

error: Content is protected !!