Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea ataja kinachoitesa CCM
Habari za Siasa

Kubenea ataja kinachoitesa CCM

Saed Kubenea
Spread the love

SAED Kubenea, Mgombea Ubunge kinondoni kupitia Chama cha ACT-Wazalendo ametaja masuala yanayokitesa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwenye kampeni za Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Kubenea ametaja sababu hizo jana Jumamosi tarehe 3 Oktoba 2020 katika mkutano wake wa kampeni Wilayani Kinondoni, Dar es Salaam.

Mwanasiasa huyo amesema, zuio la mikutano ya hadhara kwa takribani miaka mitano, kukandamizwa kwa wanasiasa wa upinzani, kuzuia mikutano ya bunge kurushwa mubashara, ndio kinachowapa shida CCM wakati huu.

“Ndio maana Rais John Magufuli  na chama chake kinapata shida sana katika uchaguzi huu,  walizuia mikutano ya hadhara miaka mitano, wakauzia bunge live, wakazuia wabunge wao wasiseme bungeni, wakakamata wapinzani na kuwafungulia kesi,  wakanunua wabunge wa upinzani, wakifikiri shughuli imeisha kumbe ndio kwanza inaanza,” amesema Kubenea.

Kubenea amewaomba wananchi wa Kinondoni wamchague badala ya kuchagua Mgombea wa CCM, Abbas Tarimba akisema, wabunge wa upinzani wana uwezo wa kutimiza majukumu ya mbunge ambayo ni kuisimamia, kuishauri na kuiwajibisha Serikali inapokosea.

“Kazi za mbunge ni tatu, kusimamia Serikali, maana ya kusimamia mnajua ni lazima uwe na ushupavu na ujasiri wa kusimama na kumkemea mtu, mbili kushauri Serikali, tatu kuiwajibisha,  hizo ndio kazi za mbunge ukiwa na mbunge unayetokana na CCM huwezi simamia Serikali hasa ya Magufuli, wabunge wa CCM  wote wameufyata,” amesema Kubenea.

Kubenea ambaye kitaalamu ni mwandishi wa habari alisema, yeye yuko tayari kuwawakilisha vyema wananchi wa Kinondoni kwani uzoefu huo anao na matatizo ya jimbo hilo anayajua.

Amesema, Tarimba hawezi kwenda kuwawakilisha vyema kwani ataweka mbele maslahi yake na ya chama chake jambo ambalo litawafanya wana Kinondoni kutokuwa na msemaji na mwakilishi madhubuti ndani na nje ya Bunge.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!