Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema yamuunga mkono Maalim Seif, kuachiana majimbo na kata
Habari za Siasa

Chadema yamuunga mkono Maalim Seif, kuachiana majimbo na kata

Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimetangaza kumuunga mkono Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Maalim Seif Sharif Hamad, pamoja na kuachiana majimbo na kata na chama hicho katika Uchaguzi Mkuu wa tarehe 28 Oktoba 2020. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Uamuzi huo umetangazwa leo Jumapili tarehe 4 Oktoba 2020 na Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema wakati anatangaza maazimio ya Kamati Kuu ya chama hicho, iliyoketi jana Jumamosi jijini Dar es Salaam.

Maalim Seif Sharrif Hamad, Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo

Mbowe amesema, uamuzi huo umekuja baada ya  Mgombea Urais wa Chadema Zanzibar, Said Issa Mohammed kuridhia kujitoa katika kinyang’anyiro hicho na kumuunga mkono Maalim Seif.

 

“Sisi kama Kamati Kuu jana tumeamua na kuridhika na kauli za viongozi wa vyama vyetu hususan Chadema na ACT baada ya kushauriana kwa kina na mgombea wetu wa Zanzibar tumeona ni sahihi chama chetu kumuunga mkono Maalim Seif na kwa maana hiyo anaridhia kujitoa kwa hiari yake,” amesema Mbowe

Mbowe amesema, Kamati Kuu za Chadema na ACT-Wazalendo ziko katika utaratibu wa kutafuta namna watakavyoshirikiana katika Uchaguzi wa wabunge na madiwani kwa pande zote mbili, Tanzania Bara na Zanzibar.

“Chama chetu kimeona umuhimu wa ushirikishwaji wa ngazi mbalimbali za chama katika kuungana kwenye kusimamisha wagombea wa ubunge na udiwani, tumeziachia kamati (za Chadema na ACT-Wazalendo) kufanya mazungumzo kwa haraka kuona tunaachianaje majimbo na kata,” amesema  Mbowe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

error: Content is protected !!