Tuesday , 30 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema yamuunga mkono Maalim Seif, kuachiana majimbo na kata
Habari za Siasa

Chadema yamuunga mkono Maalim Seif, kuachiana majimbo na kata

Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimetangaza kumuunga mkono Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Maalim Seif Sharif Hamad, pamoja na kuachiana majimbo na kata na chama hicho katika Uchaguzi Mkuu wa tarehe 28 Oktoba 2020. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Uamuzi huo umetangazwa leo Jumapili tarehe 4 Oktoba 2020 na Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema wakati anatangaza maazimio ya Kamati Kuu ya chama hicho, iliyoketi jana Jumamosi jijini Dar es Salaam.

Maalim Seif Sharrif Hamad, Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo

Mbowe amesema, uamuzi huo umekuja baada ya  Mgombea Urais wa Chadema Zanzibar, Said Issa Mohammed kuridhia kujitoa katika kinyang’anyiro hicho na kumuunga mkono Maalim Seif.

 

“Sisi kama Kamati Kuu jana tumeamua na kuridhika na kauli za viongozi wa vyama vyetu hususan Chadema na ACT baada ya kushauriana kwa kina na mgombea wetu wa Zanzibar tumeona ni sahihi chama chetu kumuunga mkono Maalim Seif na kwa maana hiyo anaridhia kujitoa kwa hiari yake,” amesema Mbowe

Mbowe amesema, Kamati Kuu za Chadema na ACT-Wazalendo ziko katika utaratibu wa kutafuta namna watakavyoshirikiana katika Uchaguzi wa wabunge na madiwani kwa pande zote mbili, Tanzania Bara na Zanzibar.

“Chama chetu kimeona umuhimu wa ushirikishwaji wa ngazi mbalimbali za chama katika kuungana kwenye kusimamisha wagombea wa ubunge na udiwani, tumeziachia kamati (za Chadema na ACT-Wazalendo) kufanya mazungumzo kwa haraka kuona tunaachianaje majimbo na kata,” amesema  Mbowe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

Habari za Siasa

ACT Wazalendo yaanika madudu miradi ya ujenzi, moundombinu

Spread the loveCHAMA cha ACT Wazalendo kimeeleza wasiwasi juu ya uelekeo wa...

Habari za Siasa

Samia ashuhudia utiaji saini ujenzi wa minara 758 ya bilioni 265

Spread the love  RAIS Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa kampuni za...

error: Content is protected !!