Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa IGP Sirro aonya Polisi kujihusisha na siasa
Habari za Siasa

IGP Sirro aonya Polisi kujihusisha na siasa

IGP Simon Sirro
Spread the love

MKUU wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro amewataka askari polisi kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa sheria, na kukwepa kujihusisha na masuala ya siasa. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

IGP Sirro ametuma salamu hizo leo tarehe 21 Septemba 2019, wakati akizungumza na askari polisi jijini Arusha.

IGP Sirro ameeleza kuwa, Jeshi la Polisi haliko kwenye upande wa siasa, na kuwa askari polisi wanapaswa kusimamia sheria.

“Sisi tunasimamia sheria, sisi hatuko kwenye upande wa siasa. Kwa hiyo simamia sheria zilizopo. Wajibu wetu mkubwa ni kusimamia sheria, kwa hiyo salamu zangu ni hizo,” amesema IGP Sirro.

Aidha, IGP Sirro amewataka askari polisi nchini kuwa waadilifu huku akionya wenye tabia ya kuuzia wenzao sare za polisi, akisema kwamba hatowavumilia.

“Sikuteuliwa IGP kuja kufukuza askari, kwa askari asinilazimishe kumfukuza,” amesema IGP Sirro.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!