Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Mlipuko wa bomu wauwa mmoja na kujeruhi wawili Kibaha
Habari Mchanganyiko

Mlipuko wa bomu wauwa mmoja na kujeruhi wawili Kibaha

Spread the love

MBARAKA Koromera (37) amepoteza maisha na wengine wawili kujeruhiwa katika mlipuko wa kifaa kinachodhaniwa kuwa bomu, uliotokea maeneo ya Msangani wilayani Kibaha mkoa wa Pwani. Anaripoti Hamisi Mguta…(endelea).

ACP Wankyo Nyigesa, Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani amesema tukio hilo limetokea jana tarehe 20 Septemba 2019, majira ya saa tano asubuhi.

Kamanda Nyigesa ameeleza kuwa, mlipuko huo umetokea wakati marehemu Koromera anachambua vyuma chakavu kwenye pagale la mtu aliyefahamika kwa jina la Rajab Nyangale.

Kamanda Nyigesa amewataja waliojeruhiwa kwenye mkasa huo kuwa ni, Fatuma Likupila na Shomari Athumani ambao wanapatiwa matibabu katika Hospitali ya Tumbi wilayani Kibaha.

Amesema baada ya tukio hilo kutokea, Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) lilifika eneo la tukio na kukuta vipande vitano vidhaniwazo kwamba ni mabomu, ambavyo inafanyia upelelezi.

“Katika eneo la tukio ambako Jeshi la Polisi tulifika kwa kusaidiana na JWTZ tumeokota vipande 5 vidhaniwavyo kuwa ni mabomu kwa ajili ya uchunguzi,” amesema Kamanda Nyigesa.

Kamanda Nyigesa ametoa tahadhari kwa wananchi kutohifadhi vyuma chakavu ndani ya nyumba pamoja na kutookota ovyo vifaa chakavu.

“Tunatoa rai kwa wananchi kuwa waangalifu, kuhifadhi vyuma chakavu nje ya nyumba. Na vyuma chakafu visiokotwe bila ya kupata ushauri wa watalaamu,” amesema Kamanda Nyigesa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi wa wanawake watakiwa kuchangamkia fursa za elimu

Spread the love  KAMISHNA wa Polisi Utawala Menejimenti ya rasilimali watu, CP...

Habari Mchanganyiko

Vijana 400 waguswa na programu ya “Learning for Life” ya SBL

Spread the love  PROGRAMU ya “Learning for Life” imetimiza dhamira ya Serengeti...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Stamico yafungua fursa za kiuchumi kwa makundi maalumu

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limemwaga neema kwa watu...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

error: Content is protected !!