Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa IGP Sirro aonya Polisi kujihusisha na siasa
Habari za Siasa

IGP Sirro aonya Polisi kujihusisha na siasa

IGP Simon Sirro
Spread the love

MKUU wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro amewataka askari polisi kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa sheria, na kukwepa kujihusisha na masuala ya siasa. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

IGP Sirro ametuma salamu hizo leo tarehe 21 Septemba 2019, wakati akizungumza na askari polisi jijini Arusha.

IGP Sirro ameeleza kuwa, Jeshi la Polisi haliko kwenye upande wa siasa, na kuwa askari polisi wanapaswa kusimamia sheria.

“Sisi tunasimamia sheria, sisi hatuko kwenye upande wa siasa. Kwa hiyo simamia sheria zilizopo. Wajibu wetu mkubwa ni kusimamia sheria, kwa hiyo salamu zangu ni hizo,” amesema IGP Sirro.

Aidha, IGP Sirro amewataka askari polisi nchini kuwa waadilifu huku akionya wenye tabia ya kuuzia wenzao sare za polisi, akisema kwamba hatowavumilia.

“Sikuteuliwa IGP kuja kufukuza askari, kwa askari asinilazimishe kumfukuza,” amesema IGP Sirro.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

error: Content is protected !!