Tuesday , 30 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa IGP Sirro aonya Polisi kujihusisha na siasa
Habari za Siasa

IGP Sirro aonya Polisi kujihusisha na siasa

IGP Simon Sirro
Spread the love

MKUU wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro amewataka askari polisi kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa sheria, na kukwepa kujihusisha na masuala ya siasa. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

IGP Sirro ametuma salamu hizo leo tarehe 21 Septemba 2019, wakati akizungumza na askari polisi jijini Arusha.

IGP Sirro ameeleza kuwa, Jeshi la Polisi haliko kwenye upande wa siasa, na kuwa askari polisi wanapaswa kusimamia sheria.

“Sisi tunasimamia sheria, sisi hatuko kwenye upande wa siasa. Kwa hiyo simamia sheria zilizopo. Wajibu wetu mkubwa ni kusimamia sheria, kwa hiyo salamu zangu ni hizo,” amesema IGP Sirro.

Aidha, IGP Sirro amewataka askari polisi nchini kuwa waadilifu huku akionya wenye tabia ya kuuzia wenzao sare za polisi, akisema kwamba hatowavumilia.

“Sikuteuliwa IGP kuja kufukuza askari, kwa askari asinilazimishe kumfukuza,” amesema IGP Sirro.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

Habari za Siasa

ACT Wazalendo yaanika madudu miradi ya ujenzi, moundombinu

Spread the loveCHAMA cha ACT Wazalendo kimeeleza wasiwasi juu ya uelekeo wa...

Habari za Siasa

Samia ashuhudia utiaji saini ujenzi wa minara 758 ya bilioni 265

Spread the love  RAIS Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa kampuni za...

error: Content is protected !!