CHAMA Cha Wananchi (CUF) nchini Tanzania, kimewatangaza wagombea wake 136 wa ubunge katika majimbo ya Tanzania Bara. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea)
Tanzania bara ina majimbo 214 na Zanzibar majimbo 50. Hii ina maana kwamba, bado haijateua majimnbo 76 ili kutimiza 214.
Orodha hiyo imetoelwa leo Jumatatu tarehe 24 Agosti 2020 ikiwa ni siku moja imesalia kabla ya shughuli ya uchukuaji na urejeshaji wa fomu za uteuzi kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kufungwa.
Kesho Jumanne tarehe 25 Agosti 2020, NEC itafanya uteuzi wa wagombea watakaokidhi vigezo.
Kampeni za uchaguzi huo zitaanza tarehe 26 Agosti hadi 27 Oktoba 2020 na uchaguzi mkuu utakuwa Jumatano 28 Oktoba 2020.
Orodha yote ya wagombea hii hapa;
Leave a comment